Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, February 21, 2014

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: ARSENAL 0 v BAYERN MUNICH 2, TONI KROOS NA THOMAS MULLER WAIVUNJA MOYO GUNNERS EMIRATES

Arsenal na Bayern zote zilikosa mikwaju ya penati ya ungwe ya dakika za kipindi cha kwanza lakini bao mbili za kipindi cha pili kutoka kwa Kroos na Mueller zimewapa ushindi Bayen wa bao 2-0 dhidi ya wenyeji Gunners, ambapo kipa wao Szczesny ameondoshwa kwa kadi nyekundu leo kwenye Mtanange wa UEFA Champions Ligi hatua ya 16 ya mtoano.Dakika ya nane Mchezaji wa Bayern Munich Jerome Boateng alimwangusha Ozil ndani ya eneo hatari na Mwamuzi kumpa kadi ya njano Boateng na mkwaju wa penati kupigwa...Mesut Ozil
Mkwaju huo umedakwa kwa kupanguliwa nje na kipa wa Bayern Munich Manuel Neuer uliopigwa na Mesut Ozil katika dakika ya 8. Dakika ya 37 kipindi cha kwanza kipa wa Arsenal Wojciech Szczesny anatolewa nje kwa kupewa kadi nyekundu baada ya kumfanyia ndivyo sivyo Robben ndani ya eneo hatari, Mkwaju wa penati unatengwa. David Alaba anakosa penati mpira unagonga posti na kutoka nje!! Arsenal wanafanya mabadiliko Santi Cazorla anatoka na nafasi yake inachukuliwa na kipa Lukasz Fabianski katika dakika ya 39 kipindi cha kwanza na dakika ya 31 pia Arsenal walifanya mabadiliko ya Kieran Gibbs baada ya kuumia na nafasi yake kuchukuliwa na Monreal. Kosa kosa hizo za penati katika timu zote mbili zimesababisha timu zote kwenda mapumziko 0-0.Kikosi cha Arsenal kilichoanza Kikosi cha Bayern Munich kilichoanzaKocha wa Bayern Munich Pep GuardiolaOzil baada ya kuangushwa na Jerome Boateng ndani ya 18
Mkwaju wa Ozil ukidakwa na kipa wa Bayern Munich Manuel Neuer mapema kipindi cha kwanza!Ozil akiachia shuti njaa na kudakwa na kipa wa Bayern
Sanogo akikatiza katikati ya mabeki wa BayernYaya Sanogo kwenye patashika, katika mtanange huu alianza kipindi cha kwanzaWojciech Szczesny akiokoa moja ya shuti kali langoni mwake
Kipindi cha pili dakika ya 46 Bayern Munich wanafanya mabadiliko ya Jerome Boateng na nafasi yake
kuchukuliwa na Rafinha. Dakika ya 54 kipindi cha pili Toni Kroos akaifungia bao timu yake Bayern Munich baada ya kupewa pasi  na Philipp Lahm.

Baadae kidogo Yaya Sanogo akapewa kadi ya njano baada ya kumchezea ndivyo sivyo kipa wa Bayern Munich Never. Dakika za
lala salama dakika ya 88 mchezaji wa Bayern Munich Thomas 
Müller aliyetokea benchi  akaifungia bao timu yake, Bao la kichwa baada ya kupewa pasi safi na Philipp Lahm.David Alaba nae alikosa penati hivi hivi...!
Kipa Szczesny akiruka na Arjen Robben...Nje!!!Robben akijiuguza kama vile katolewa ulimi!!.....uko sawa?? nyanyuka sasa!!
Kweli unamtoa nje???Kipa Lukasz Fabianski alichukua nafasi ya Santi CazorlaThomas Mueller akimpa tano Lahm!
VIKOSI:
Arsenal: Szczesny, Sagna, Mertesacker, Koscielny, Gibbs, Flamini, Wilshere, Oxlade Chamberlain, Ozil, Cazorla, Sanogo. Subs: Fabianski, Rosicky, Podolski, Giroud, Monreal, Jenkinson, Gnabry.
Bayern Munich: Neuer, Lahm, Boateng, Dante, Alaba, Thiago, Javi Martinez, Robben, Kroos, Gotze, Mandzukic. Subs: Starke, Van Buyten, Rafinha, Pizarro, Muller, Contento, Schweinsteiger.
Mwamuzi:Nicola Rizzoli (Italy)

No comments:

Post a Comment