Mchezaji huyo aliyeichezea watani wa Swansea, Cardiff City alizomewa kupitia kiupindi chote cha mchuano na mashabiki wa Swansea.
Bao la Ramsey lilipatikana katika dakika ya 62 kuipa klabu yake ya Arsenal mabao mawili kuthibitisha mwendo wao wa kushinda.
Ushindi wa Arsenal umeizidishia klabu hiyo rekodi ya kushinda ugenini kutimiza mechi 12 ikiwa ni sawa na rekodi yao ya mechi nane katika Ligi ya Premier iliyowekwa katika msimu wa mwaka 2001-02.
Katika ushindi wa jumamosi, Ramsey, aliyejiunga na Arsenal mwaka 2008 akiwa kija na mwenye umri wa miaka 17 na baada ya hapo kukumbwa na jeraha lililomueka nje ya mchezo ka kipindi kirefu na baada ya hapo kushindwa kufikia viwango na kukemewa na mashabiki hapo jana alikua chachu ya ushindi dhidi ya Swansea.
No comments:
Post a Comment