Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, February 14, 2018

UHURU FM YAJA NA MIC TATA

Uhuru FM kwa kushirikiana na Dar-live itafanya show inayokwenda kwa jina la MIC TATA itakayokutanisha miamba ya Muziki nchini.
Mratibu show hiyo Said Ambua, amesema Wasanii watakaokutanishwa katika shown hiyo ya MIC TATA ni wa Bongo Flava, Singeli, Taarabu na Hip Hop.
Aliwataja wasanii hao  kuwa ni Barnaba, Inspector Horun, Manfongo, Dulla Makabila, Joh Makini, ambapo kwa upande wa taarabu ni Amigo ambaye alikuwa kwenye band ya Mzee Yusuph na kwa sasa anajitengemea.
Alisema lengo la Show hiyo ni muendelezo wa kampeni ya GUSA MAISHA YAO ambayo inalengo la kusaidia wasiojiweza kwa kile kitakachopatikana.
Show hiyo itafanyika katika ukumbi wa Dar-Live, Mbagala Zakyeem Februari 24 Mwaka huu kwa kiingilio cha shilling 5,000 kuanzia saa mbili za usiku.
Kampeni ya Gusa Maisha Yao ilianza mwaka jana kwa kituo cha Uhuru Fm kutoa msaada katika Hospitali ya Taifa Muhimbili, kuchangia damu, na kutoa msaada kituo cha waathirika wa dawa za kulenya.


No comments:

Post a Comment