Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, April 24, 2017

NYOTA IMARA ZAIDI WA SOKA ULAYA



WIKI iliyopita tulishuhudia mechi kali Ulaya, ambapo miamba ilikuwa ikipambana kutafuta kufuzu kuingia nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (UCL).
Waliovuka wamefanya hivyo, hata kama ni kwa malalamiko ya waliokwama, na sasa tutasubiri kuina nusu fainali. Wakati tukisubiri hayo, tunaendelea kusawiri ni wachezaji gani vijana walio mahiri sana kwa sasa Ulaya hii hii.
Image result for Niklas Sule
Niklas Sule (Hoffenheim, 21, Mlinzi) 

Kwa kawaida ukiona Bayern Munich wamemfuata mchezaji na kumng’ang’ania katika soka ya Ujerumani basi ujue hicho kweli ni kifaa. Miamba hawa wa Ujerumani walijihisi kwamba walitakiwa kuisaka kwa udi na uvumba saini ya Niklas Sule kwa ajili ya msimu ujao, na tayari wameshafanya hivyo.
Wanadaiwa kumfunga mkataba wa muda mrefu kwa thamani ya pauni milioni 21.68, Ni rahisi kuona sababu; akiwa na umri wa miaka 21 tu tayari Sule amejiongeza kuwa mmoja wa walinzi bora zaidi wa kati katika Bundesliga.
Kocha wa Timu ya Taifa ya Ujerumani, Joachim Low hakushindwa kumuona na tayari amemchezesha kimataifa wakati katika ngazi ya klabu Sule ametoa mchango mkubwa kwa Hoffenheim kujisukuma kuendea nafasi za juu za ligi kuu.
Sule ni mbichi, akiwa na sehemu ya kuongeza vitu bado kwa ajili ya kujiboresha yeye na timu atakazokuwa nazo; ni aina ya mlinzi wa kisasa anayeonesha mahaba kwa mpira kuwa mguuni pale lakini pia ni mzuri angani na ana nguvu za miguu na kichwa na anafaa kwa mfumo wa kocha yeyote yule.


Image result for Alexander Isak
Alexander Isak (Borussia Dortmund, 17, Mshambuliaji)

Uliza mshambuliaji yeyote ni mshambuliaji gani wangependa kufananishwa naye, basi Zlatan Ibrahimovic atakuwa juu miongoni mwao. Alexander Isak anatambulika katika Ujerumani kama ‘The Zlatan’ mpya. Alilazimisha kuingia kikosi cha kwanza akiwa na umri wa miaka 16 tu na alipofikisha umri wa miaka 17 alikuwa anaongoza mstari wa mashambulizi akiwa na AIK, akafunga bao dakika ya 15 tu siku yake ya kuzaliwa.
Uwapo wake uwanjani unasikika sana, yupo vizuri akiwa na mpira na muda wote hufungua vyumba tayari kuupokea. Mchezaji huyu aliyezaliwa Sweden na wazazi raia wa Eritrea ni mmaliziaji mzuri ambaye mwaka jana alifunga mabao 10 akiwa Ligi Kuu ya Sweden. Haikushangaza kuona kwamba Real Madrid ni moja ya klabu zilizomtaka ila ameamua kuwa na Dortmund mwaka huu, na amefanya vyema kwani atapata muda zaidi wa kucheza.
Image result for Sandro Ramirez

Sandro Ramirez (Malaga, 21, Mshambuliaji)

Ikiwa Alexander Isak anataka uthibitisho kwamba alifanya uamuzi sahihi, amtazame tu Sandro Ramirez. Mshambuliaji huyu Mhispaniola alipanda kutoka Akademia ya Barcelona – La Masia – lakini akaachwa tu akizurura kutokana na marufuku ya usajili waliyowekewa.
Kiangazi kilipofika aliamua kuondoka akajiunga na Malaga akiwa mchezaji huru na mambo yamemwendea vizuri kabisa. Katika mechi 19 amefunga mabao saba kwenye Ligi Kuu ya Hispania, ameiva vile ambavyo Barcelona wangependa.
Angeweza kuingia Ligi Kuu ya England (EPL) maana tayari Kocha wa Tottenham Hotspur, Mauricio Pochettino alimuwinda mara kadhaa. Huenda Malaga wakikubali Pochettino angemchukua kiangazi kijacho.
 Image result for Morgan Sanson

Morgan Sanson (Marseille, 22, Kiungo)

Kifaa kilichosukwa hasa hiki na kimekuwa kkipamba vichwa vya habari, ikiwa ni zaidi ya Dimitri Payet aliyesajiliwa kutoka West Ham. Utampenda ukimwona anavyocheza kwenye Uwanja wa Stade Velodrome.
Sanson ameshacheza mechi 146 kwenye timu ya wakubwa kwa umri wake huo mdogo tu na kwa hakika ni mtu mwenye ubunifu mkubwa. Marseille walimpata kwa euro milioni tisa tu. Alikuwa mchezaji wa kwanza katika Ligue 1 ya Ufaransa kutoa usaidizi kwa mabao 10 msimu huu,idadi kubwa kwa kiungo wa kati.
Kila wiki anazidi kuwa bora kwa klabu yake ambapo kwa wiki tano kwenye mechi sita ama amefunga bao au kutoa usaidizi kwa jamaa hawa wanaojulikana kwa jina la utani la Les Phoceens.
 Image result for Jose Luis Gaya
 Jose Luis Gaya (Valencia, 21, Beki wa Kushoto)

Manchester City wana matatizo kwenye ngome yao na moja ya suluhu kwao ingekuwa kumpata mtu wa aina ya Jose Luis Gaya. Ni beki mwenye akili ya kushambulia na amewasaidia sana Valencia katika La Liga.
Gaya ana kasi lakini licha ya umbo lake dogo amekuwa akiwazidi kimsuli mawinga wakubwa kwa umbo. Kuna uwezekano mkubwa kabisa kwa Gaya kuwa mzuri zaidi lakini tayari ameonesha vitu adimu na Pep Guardiola anaweza kuwa kocha mwenye kumhitaji na kumfaidi zaidi, ambapo ana uwezo wa kuwaimarisha walinzi wadogo kuwa bora kabisa duaniani.
 Image result for Giovanni Simeone
Giovanni Simeone (Genoa, 21, Mshambuliaji)

Kuingia Ulaya kunaweza kuwa kugumu kwa mchezaji mdogo, lakini huweza kumsaidia ikiwa ana familia huku. Hii ndiyo hali aliyo nayo Giovani ‘Cholito’ Simeone, mwana wa Kocha wa Atletico Madrid, Diego Simeone.
Someone alionesha uzuri wake mapema msimu huu alipofunga bao dhidi ya mabingwa wa Italia, Juventus na kuwapa Genoa ushindi murua sana uliofurahiwa. Amefunga mabao 10 katika mechi 20 alizocheza hadi naandika mhaya.
Hii maana yake ni kwamba anaanza kuwavuta klavu kubwa kutoka nchi mbalimbali, ikiwa ni pamoja na England, kumtaka. Ana nguvu sana, mchezo mzuri lakini pia anajua cha kufanya wakati hana mpira. Inaelezwa kwamba Everton wanalenga kumsajili, lakini hata kama si kweli huu ni mwanzo tu wa mshambuliaji anayetarajiwa kuwa mahiri kuliko hata baba yake. ITAENDELEA.

No comments:

Post a Comment