Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, October 4, 2016

JOSE MOURINHO ALIA NA RATIBA MAN UNITED , MECHI 5 NDANI YA SIKU 13 DHIDI YA LIVERPOOL, FENERBAHCE, CHELSEA, CITY, BURNLEY


MENEJA wa Manchester United Jose Mourinho ameielezea Ratiba yao kuwa ni ‘zawadi yenye sumu’.
Baada ya hii Vakesheni ya EPL, Ligi Kuu England, kupisha Mechi za Kimataifa zilizomo kwenye Kalenda ya FIFA na Ligi kurejea tena Wikiendi ya Oktoba 15, Man United watacheza Mechi 5 ndani ya Siku 13 kuanzia Jumatatu Oktoba 17.

Mourinho, akishangazwa na upangaji wa Ratiba wa wao kucheza na Mahasimu wao Jumatatu Oktoba 17 badala ya Siku 2 kabla wakati Siku 3 baadae watakutana na Fenerbahce kwenye Mechi ya UEFA EUROPA LIGI, ameeleza: “Sawa, tungeweza kucheza na Liverpool Jumamosi [Okt 15], tungeweza kucheza na Liverpool Jumapili [Okt 16] lakini tunacheza na Liverpool Jumatatu [Okt 17]! Pengine hatuna mazingira mazuri kwani tutacheza na Timu za juu 2 za EPL ambazo hazipo Ulaya!”

Msimu huu, Liverpool na Chelsea hawamo kwenye Mashindano yeyote ya UEFA ya Ulaya na hivyo hawachezi Kati-Wiki tofauti na Man United ambao wapo UEFA EUROPA LIGI. Baada ya kucheza na Liverpool Jumatatu Oktoba 17 huko Anfield, Alhamisi Oktoba 20 Man United watacheza na Fenerbahce Old Trafford na Jumapili Oktoba 23 wako huko Stamford Bridge kuivaa Timu ya zamani ya Mourinho Chelsea na kurejea tena Old Trafford Jumatano Oktoba 26 kuivaa Man City.

Mourinho ameeleza: “Tunayo hii zawadi yenye sumu ya kucheza Jumatatu ambayo inaleta shida kubwa lakini tunataka kufuzu na inabidi tupange Kikosi kinachoweza kuifunga Fenerbahce.”

Kwenye EUROPA LIGI, katika Kundi A, Man United wako Nafasi ya 3 wakiwa Pointi 1 nyuma ya Vinara Fenerbahce na wao wakifungana Pointi na Feyenoord ambao ni wa Pili.

Mourinho anahisi hawana la kufanya na kutamka: “Nadhani haiwezekani. Zawadi yenye sumu ipo. Tutafanyaje? Inabidi tucheze Jumatatu na kisha Alhamisi na ikifuata Stamford Bridge Jumapili!”

MAN UNITED – Mechi zao:
October 2016

EPL, Ligi Kuu England
Jumatatu Oktoba 17
2200 Liverpool v Man United

UEFA EUROPA LIGI - Kundi A
Alhamisi Oktoba 20
2205 Man United v Fenerbahçe

EPL, Ligi Kuu England
Jumapili Oktoba 23

1800 Chelsea v Man United

EFL Cup – Raundi ya 4
Jumatano Oktoba 26

2200 Man United v Man City

EPL, Ligi Kuu England
Jumamosi Oktoba 29

1700 Man United v Burnley

November 2016
UEFA EUROPA LIGI - Kundi A


Alhamisi Novemba 3
2100 Fenerbahçe v Man United

EPL, Ligi Kuu England
Jumapili Novemba 6

1800 Swansea v Man United

EPL, Ligi Kuu England
Jumamosi Novemba 19

1530 Man United v Arsenal

UEFA EUROPA LIGI - Kundi A
Alhamisi Novemba 24

2305 Man United v Feyenoord

EPL, Ligi Kuu England
Jumapili Novemba 27

1930 Man United v West Ham

December 2016
EPL, Ligi Kuu England
Jumamosi Desemba 3

1800 Everton v Man United

UEFA EUROPA LIGI - Kundi A
Alhamisi Desemba 8

2100 Zorya Luhansk v Man United

EPL, Ligi Kuu England
Jumapili Desemba 11

1800 Man United v Tottenham

EPL, Ligi Kuu England
Jumatano Desemba 14

2300 Crystal Palace v Man United

EPL, Ligi Kuu England
Jumamosi Desemba 17

1800 West Brom v Man United

EPL, Ligi Kuu England
Jumatatu Desemba 26

1800 Man United v Sunderland

EPL, Ligi Kuu England
Jumamosi Desemba 31 

1800 Man United v Middlesbrough

No comments:

Post a Comment