Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, October 6, 2016

ABDUL MOHAMED AWA MENEJA WA AZAM FC NA FARID MUSA KUONDOKA MUDA WOWOTE KWENDA HISPANIA




Mkurugenzi Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba akizungumza na wandishi wakati wa kumtambulisha Abdul Mohamed ambaye ni Meneja mkuu wa Azam FC
UONGOZI wa Azam FC, umesema umeshatuma uhamisho wa kimataifa (ITC) wa Farid Mussa nchini Hispania lakini kibali cha kufanya kazi ndio kinamkwamisha kuondoka nchini.
Akizungumza na wandishi wa habari, Mkurugenzi Mkuu wa Azam FC, Saad Kawemba alisema Azam wameshawatumia hati ya uhamisho ya kimataifa (ITC) kwa klabu ya Tenerrife inayoshiriki ligi daraja la kwanza ambayo imekuwa ikihitaji huduma za winga huyo
“Suala la Farid lipo kwenye hatua nzuri muda si mrefu winga huyo ataelekea nchini Hispania kwakua kila kitu kinaenda sawa, tunasubiri kibali cha kazi kikipatikana hata kesho anasafiri,"
Pia Kawemba alisema hawezi kumkwamisha Farid kucheza soka la kulipwa kwa sababu wamempeleka kwa mkopo na ndio wanagharamia kila kitu kwa makubaliano ambayo wamewekeana na klabu ya Tenerrife kuwa watakuwa wanapeleka wachezaji na wao watakuwa wanawaleta wachezaji Azam FC.
Kawemba alitolea ufafanuzi swala la timu yao kuvaa nembo ya mdhamini wa ligi kuu Tanzania bara kwenye mkono mmoja na kudai wakati wanatisha kanuni ilisemekana timu ikipata mdhamini itumie mkono huo mwingine hivyo na wao wamepata mdhamini mwingine.
“Kwanza sijapata barua kuwa tumepigwa faini na shirikisho la soka Tanzania (TFF) na endapo tutapata tutaeleza sababu ya sisi kutovaa maana lakini kwenye viwanja kuna matangazo ya wadhamini ambayo klabu hazina taarifa zake”, alisema Kawemba.
Kawemba alifika mbali na kusema hiyo kanuni ya kuvaa nembo ya mdhamini kwenye mikono yote iondolewe kama ilivyoondolewa kanuni ya mchezaji mwenye kadi nyekundu kuchagua mchezo wa kucheza.
Wakati huo huo, Kawemba amemtambulisha Abdul Mohamed kuwa Meneja Mkuu wa Azam FC, ajira ambayo ameanza kuitumikia kuanzia Septemba.
Kawemba alisema wamemchukua Mohamed ili kuboresha klabu yao kwenye ushindani wa uwanjani na nje ya uwanja kwani soka kwa sasa ni biashara kubwa duniani.
Naye Mohamed ambaye kitaaluma ni mwandishi wa habari na mtaalamu wa Fedha, Uhasibu na Uchumi alisema amefurahi kuwa familia ya Azam na kuomba ushirikiano ili kufanikisha majukumu ya kila siku.

No comments:

Post a Comment