Mmiliki wa Leicester City ambaye pia ni mfanya biashara kutoka Thailand, Vichai Srivaddhanaprabha amewapa wachezaji 30 wa kikosi cha Leicester City gari aina ya Mercedes B-Class zilizo na thamani ya Pauni 32,670 sawa na Milioni 103 za kitanzania kila mmoja ikiwa ni zawadi ya kutwaa ubingwa la Ligi Kuu ya Uingereza kwa mara ya kwanza.
33CB8D0300000578-3574048-image-m-4_1462397114208
Wachezaji wa Leicester City wakishangilia ubingwa wa Ligi Kuu ya Uingereza.
Kwa mujibu wa mtandao wa Sportsmail umeeleza kuwa baada ya Srivaddhanaprabha kutoa zawadi hiyo, itamgharimu kiasi cha Pauni Milioni moja kuwanunulia wachezaji wote 30 aina hiyo ya magari.
Aidha tayari bilionea huyo ameshakiahidi kikosi cha Claudio Ranieri kuwa atagharamia gharama za kuwapeleka Las Vegas ikiwa ni sehemu ya kusherekea mafanikio waliyopata msimu wa 2015/2016.