

Halmashauri
ya Jiji la Liverpool limeipa Klabu ya Liverpool Kibali cha ujenzi ambao
utawawezesha kupanua Jukwaa Kuu la Uwanja huo na kuchukua Watu 8,300
zaidi na Jukwaa la Barabara ya Anfield kuongezwa na kubeba Watu 4,800
zaidi.
Upanuzi wa Anfield unatarajiwa kuanza Mwakani na kukamilika kabla ya Msimu wa 2016/17.
Mapendekezo ya Liverpool ya upanuzi wa Uwanja huo yanahusu kulifanya Jukwaa Kuu liwe na ngazi mbili za Watazamaji wanaokaa Vitini na pia kuongeza sehemu za Mikutano na Hoteli, sehemu za Duka la Klabu na kupanua sehemu ya kuegesha Magari.
Katika Maombi yao ya upanuzi wa Anfield, Klabu ya Liverpool ilisema upanuzi huo umelenga Klabu yao kuweza kuwa Wenyeji wa Mashindano makubwa ya Kimataifa na Fainali za Ulaya.
Klabu hiyo ilieleza hivi sasa Anfield iko chini ya Viwango vya UEFA na Ligi Kuu England ambavyo vimeizuia Klabu hiyo kuwa Wenyeji wa Mashindano makubwa.
Mojawapo ya Viwango vya UEFA kwa Uwanja kupewa Mechi za Kimataifa ni uwezo wa Uwanja kuchukua Watu si chini ya 50,000 na kuwa na sehemu za kuridhisha za Watu muhimu pamoja na Vyumba vya Kubadili Jezi kwa Wachezaji na Marefa veynye kukidhi mahitaji ya msingi kwa viwango maalum.
Hata hivyo uamuzi huu wa Halmashauri ya Jiji la Liverpool kuipa Klabu ya Liverpool Kibali cha ujenzi umezua upinzani toka baadhi ya Wananchi wa Jiji la Liverpool wanaodai upanuzi huo utalichafua Jiji na kuzidisha msongamano.
VIWANJA VINGINE VINAVYOONGOZA KWA KUINGIZA WATU WENGI LIGI KUU ENGLAND NI KAMA:
Upanuzi wa Anfield unatarajiwa kuanza Mwakani na kukamilika kabla ya Msimu wa 2016/17.

Mapendekezo ya Liverpool ya upanuzi wa Uwanja huo yanahusu kulifanya Jukwaa Kuu liwe na ngazi mbili za Watazamaji wanaokaa Vitini na pia kuongeza sehemu za Mikutano na Hoteli, sehemu za Duka la Klabu na kupanua sehemu ya kuegesha Magari.

Katika Maombi yao ya upanuzi wa Anfield, Klabu ya Liverpool ilisema upanuzi huo umelenga Klabu yao kuweza kuwa Wenyeji wa Mashindano makubwa ya Kimataifa na Fainali za Ulaya.
Klabu hiyo ilieleza hivi sasa Anfield iko chini ya Viwango vya UEFA na Ligi Kuu England ambavyo vimeizuia Klabu hiyo kuwa Wenyeji wa Mashindano makubwa.

Mojawapo ya Viwango vya UEFA kwa Uwanja kupewa Mechi za Kimataifa ni uwezo wa Uwanja kuchukua Watu si chini ya 50,000 na kuwa na sehemu za kuridhisha za Watu muhimu pamoja na Vyumba vya Kubadili Jezi kwa Wachezaji na Marefa veynye kukidhi mahitaji ya msingi kwa viwango maalum.
Hata hivyo uamuzi huu wa Halmashauri ya Jiji la Liverpool kuipa Klabu ya Liverpool Kibali cha ujenzi umezua upinzani toka baadhi ya Wananchi wa Jiji la Liverpool wanaodai upanuzi huo utalichafua Jiji na kuzidisha msongamano.
VIWANJA VINGINE VINAVYOONGOZA KWA KUINGIZA WATU WENGI LIGI KUU ENGLAND NI KAMA:
1. 75,731 - Old Trafford, Manchester United
2. 60,362 - Emirates Stadium, Arsenal
3. 52,405 - St James' Park, Newcastle United
4. 48,707 - Stadium of Light, Sunderland
5. 46,708 - Etihad Stadium, Manchester City
6. 45,522 - Anfield, Liverpool
2. 60,362 - Emirates Stadium, Arsenal
3. 52,405 - St James' Park, Newcastle United
4. 48,707 - Stadium of Light, Sunderland
5. 46,708 - Etihad Stadium, Manchester City
6. 45,522 - Anfield, Liverpool
No comments:
Post a Comment