Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, November 6, 2013

UEFA CHAMPIONS LEAGUE: BORUSSIA DORTMUND vs ARSENAL, CHELSEA vs SCHALKE 04, ARSENAL UGENINI...CHELSEA NYUMBANI DARAJANI

Klabu za England, Chelsea na Arsenal, kupambana leo na wapinzani kutoka Bundesliga huko Germany. 
Chelsea watacheza kwao Stamford Bridge na FC Schlake 04, Timu ambayo waliicharaza bao 3-0 huko Veltins Arena, Mjini Gelsenkirchen, Germany hapo Oktoba 22, na Arsenal wako Ugenini kurudiana na Borussia Dortmund ambayo iliipiga Arsenal 2-1 Uwanjani Emirates hapo Oktoba 22. Kwenye Makundi ambayo wamo Arsenal na Chelsea, mambo bado magumu na labda mwelekeo utaonekana baada Mechi za 4 kumalizika.
Arsenal wako Kundi F ambalo Vinara ni Borussia Dortmund wakifuatia Arsenal kisha Napoli lakini Timu zote hizi zina Pointi 6 kila mmoja na Marseille yuko mkiani akiwa hana hata Pointi.
Arsenal wanatinga kwenye Mechi na Borussia Dortmund wakiwa ni Vinara wa Ligi Kuu England kwa Pointi 5 mbele baada ya hivi Juzi kuifunga Liverpool Bao 2-0. 

Chelsea wako Kundi E wakiongoza na Pointi 6 sawa na Schlake na Nafasi ya Tatu ni FC Basel wenye Pointi 4 na mkiani ni Steau Bucharest wenye Pointi moja tu.

Chelsea wanacheza na Schalke huku wakitoka kwenye kipigo kwenye Ligi Kuu England baada ya Jumamosi kupigwa 2-0 na Newcastle kitu ambacho kimemkasirisha Meneja wa Jose Mourinho ambae amewaonya Wachezaji wake kuacha uzembe na pia kudaiwa kumpigwa kwanja Beki wa Brazil David Luiz. 

Mechi nyingine kubwa ni huko Nou Camp Mjini Barcelona Nchini Spain ambako Mabingwa wa Spain, FC Barcelona, watakaporudiana na AC Milan ambao walitoka nao 1-1 Wiki mbili zilizopita.
Barcelona, ambao wamepoteza Pointi 2 baada kwenda Sare ya Bao 1-1 na AC Milan kwenye Kundi H, wanaweza kufuzu ikiwa wataifunga AC Milan Uwanjani Nou Camp hapo Jumatano na matokeo mengine kwenye Kundi kuwa mazuri kwao.
 Ashley Cole wa Chelsea akifurahia jambo na Cesar Azpilicueta wakati wa mazoezi yao jana tayari kuumana na Schalke 04 usiku huu.Ashley Cole na  Gary Cahill wakati wa mazoezi yao kujiweka sawa tayari kwa mpambano usiku huu.Juan Mata wa Chelsea nae alikuwemo kwenye kikosi hicho kilichokuwa kikijifua kwenye mazoeziFrank Lampard  nae ndani!Demba Ba nae yumo leo kwenye kikosi hichoKocha Jose Mourinhoakiangalia vijana wake ambapo leo watacheza mchezo wa marudiano usiku wa leo jumatano saa 4:45.

Jumatano 6 Nov 2013 
FC Basel 1893 v FC Steaua Bucureşti
Chelsea FC v FC Schalke 04
Borussia Dortmund v Arsenal FC
SSC Napoli v Olympique de Marseille
Football Club Zenit v FC Porto [Saa 2 Usiku]
Club Atlético de Madrid v FK Austria Wien
AFC Ajax v Celtic FC
FC Barcelona v AC Milan

No comments:

Post a Comment