Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, September 30, 2013

LIVERPOOL ILIVYOICHAPA SUNDELAND 3-1 KWENYE ENGLISH PREMIER LEAGUE, KOCHA MPYA WA SUNDERLAND AKARIBISWA KWA KICHAPO



Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers (kushoto) akisalimiana na kocha mpya wa Sunderland  Kevin Ball kabla ya MtanangeDaniel Sturridge ndiye aliyeanza kuifungia bao Liverpool dakika ya 28 kipindi cha kwanza, bao safi la kiaina kwa kutupia kwa kichwa.Daniel Sturridge akishangilia bao lake la 7 kwa msimu huu.
Daniel Sturridge akiwaamusha mashabiki ugenini..
Luis Suarez nae akifurahia bao lake la pili kwa msimu huu baada ya kurudi tangu kufungiwa kwake mechi 10 na hapa aliifungia bao Liverpool dakika ya 36 kipindi cha kwanza baada ya kupewa krosi safi kama kona na kuteleza na mpira hadi nyavuni.Dakika ya 89 Luis Suarez akaongeza bao la tatu na la mwisho huku likiwa bao lake la pili kwenye mtanange huu. Ushindi huu wa Majogoo Liverpool unawapandisha juu kwenye msimamo hadi nafasi ya pili chini ya Arsenal wakiwa na Pointi 13 na Arsenal 15, Wao Sunderland ambao wamechapwa tena leo hii wamezidi kukandamizwa mkiani wakiwa na pointi 1 tu na madeni ya mabao yakiongezeka, hakika Kocha mpya anakazi ya ziada. Kesho Jumatatu usiku saa 4:00 ni Everton na Newcastle United.

No comments:

Post a Comment