![](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/09/29/1380467485396_lc_galleryImage_Liverpool_manager_Brendan.JPG)
Kocha wa Liverpool Brendan Rodgers (kushoto) akisalimiana na kocha mpya wa Sunderland Kevin Ball kabla ya Mtanange
![](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/09/29/1380469836358_lc_galleryImage_Sep_29th_2013_Sunderland_.JPG)
Daniel
Sturridge ndiye aliyeanza kuifungia bao Liverpool dakika ya 28 kipindi
cha kwanza, bao safi la kiaina kwa kutupia kwa kichwa.
![](http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2013/09/29/1380469902412_lc_galleryImage_Liverpool_s_Daniel_Sturri.JPG)
Daniel Sturridge akishangilia bao lake la 7 kwa msimu huu.
![](http://assets.espn.go.com/design05/images/2013/0929/danielsturridgecelebsunderlandliverpool_576x324.jpg)
Daniel Sturridge akiwaamusha mashabiki ugenini..
Luis Suarez nae akifurahia bao lake la pili kwa msimu huu baada ya
kurudi tangu kufungiwa kwake mechi 10 na hapa aliifungia bao Liverpool
dakika ya 36 kipindi cha kwanza baada ya kupewa krosi safi kama kona na
kuteleza na mpira hadi nyavuni.
Dakika
ya 89 Luis Suarez akaongeza bao la tatu na la mwisho huku likiwa bao
lake la pili kwenye mtanange huu. Ushindi huu wa Majogoo Liverpool
unawapandisha juu kwenye msimamo hadi nafasi ya pili chini ya Arsenal
wakiwa na Pointi 13 na Arsenal 15, Wao Sunderland ambao wamechapwa tena
leo hii wamezidi kukandamizwa mkiani wakiwa na pointi 1 tu na madeni ya
mabao yakiongezeka, hakika Kocha mpya anakazi ya ziada. Kesho Jumatatu
usiku saa 4:00 ni Everton na Newcastle United.
No comments:
Post a Comment