Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, December 13, 2012

-Wenger, Bould kuna mpasuko, mastaa Arsenal hawataki kucheza mfumo kama wa Barca


London, England

KIMENUKA! Hilo ndilo neno unaloweza kuanza kulitamka wakati ukielezea hofu kubwa ya wachezaji nyota wa Arsenal ambao wamebaini kuwepo mpasuko katika chumba chao cha kubadilishia kati ya Kocha Mkuu, Arsene Wenger na Msaidizi wake, Steve Bould.

Hali hiyo imebainika katika mechi ya Kombe la Ligi maarufu kama 'Capital One Cup' dhidi ya Bradford ambapo timu hiyo ilitolewa kwa penalti 3-2 kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 120.

Licha ya nyota hao wa Arsenal kujitahidi kucheza soka la kuvutia, wakati wa mapumziko, Wenger aliwakoromea akidai walishindwa kumudu staili hiyo ya uchezaji.

Kocha huyo pia alimpondo Gervinho kwa kukosa nafasi katika kipindi cha kwanza, lakini yote kwa yote ni wachezaji hao kubaini mpasuko kati ya Wenger na Bould ambaye alitua 'The Gunners' katika majira ya joto kuziba nafasi ya Pat Rice.

Chanzo kimoja kilisema: “Kunaonekana hakuna mawasiliano makubwa kati ya wawili hao. Ni aibu kwa sababu wachezaji wote wanaonekana kuwa nyuma ya Wenger, ingawa pia mambo ni sawa kwani wote wanamkubali Bould. Mambo yanatia hofu.”

Chanzo hicho kilieleza kuwa, Wenger bado ndiye kiongozi mkuu wa wachezaji. Kikaongeza: “Bould anawanoa mabeki kabla hata ya kuanza kwa msimu, lakini hajawahi kuruhusiwa kufanya maamuzi, Wenger amekuwa akiamua kila kitu.”

Hilo limewafanya wengi waamini usemi wa nyota wa zamani wa Arsenal, Stewart Robson, ambaye alimuita Wenger  "dikteta".

Hata hivyo, wachezaji hao pia wamemtaka Wenger kubadili mfumo wa uchezaji wa soka la kuvutia kama Barcelona na kucheza soka la nguvu na lakushtukiza.

Gazeti la "The Sun", limeeleza kuwa, wachezaji wa kikosi cha kwanza wameonekana kuwa wanyonge kutokana na kulazimishwa kucheza soka la kuvutia ambalo mara nyingi linawanyima fursa ya kupiga mashuti na hata kushindwa kuingia kwenye 18.

Chanzo hicho kilisema: “Arsenal huwa inacheza soka zuri, lakini haliwezi kuwa na mvuto kama la Barcelona.

“Mbali na hilo, pia wachezaji wanataka kazi ya kupanga safu ya ulinzi ibaki mikononi mwa Bould, huku pia wakishangaa kwanini Gervinho anaruhusiwa kucheza kama mshambuliaji wa kati wakati wengine wakilazimishwa kucheza nafasi zisizo zao.”

No comments:

Post a Comment