Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, December 5, 2012

MWAKALEBELA AJA NA UHURU DAR CORPORATE BONANZA

TIMU ya soka ya waandishi wa habari za michezo nchini ni miongoni mwa timu nane zitakazoshiriki bonanza la kusheherekea miaka 51 ya uhuru wa Tanganyika litakalofanyika kwenye viwanja vya Gymkhana jijini Dar es Salaam Desemba 9 mwaka huu kuanzia saa mbili asubuhi.

Mwenyekiti wa TASWA Majuto Omary alisema kuwa walipata barua toka Mkurugenzi wa kampuni ya Vennedrick (T) Limited kupitia Mkurugenzi wake Fredrick Mwakalebela na wameshathibitisha kuwa watashiriki.

Bonanza hili linameandaliwa na kampuni ya Vennedrick (T) Limited na litachezwa kwa mtindo wa ligi na timu mbili toka kila kundi zitafuzu hatua ya nusu fainali na limedhaminiwa na NMB banki na sasa wachezaji wa TASWA wapo kwenye maandalizi.

Timu za Barrick, NMB, DSTV na Radio Times zipo kundi A na TASWA FC, Jubilee, Azam Group na wenyeji Gymkhana wapo kundi B

Mwakalebela amesema kuwa mshindi wa kwanza, wa pili na watatu watapata zawadi na lengo la mashindano haya mbali na kuadhimisha miaka 51 ni kutumia fursa kujadili masuala mbalimbali ya michezo, matatizo na maendeleo na nini kifanyike.
 

No comments:

Post a Comment