Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, December 13, 2012

JKT OLJORO USIPIME, YAICHAKAZA KAGERA SUGAR KARUME


Mshambuliaji wa JKT Oljoro Robert Mjata akipiga shuti golini mwa Kagera Sugar wakati wa mchezo wao wa mashindano ya Uhai uliochezwa leo asubuhi uwanja wa Karume, JKT Oljoro walishinda mabao 3-0.

Benchi la JKT Oljoro B

Benchi la Kagera Sugar B

TIMU B ya JKT Oljoro leo imeanza vema mashindano ya Uhai baada ya kuifunga Kagera Sugar mabao 3-0 kwenye mchezo uliochezwa uwanja wa Karume jijini Dar es Salaam.

Mchezo huo ulikuwa wa ushindani sana na timu zote kushambuliana lakini wakichunga lango lao ulipelekea kipindi cha kwanza kumalizika bila kufungana.

Kipindi cha pili kilianza kwa timu zote kufanya mabadiliko lakini mabadiliko yaliinufaisha JKT Oljoro kwani iliweza kuifunga Kagera mabao ya haraka na kuanza kulinda lango lao.

Mabao ya JKT Oljoro yalifungwa na Hamis Swalehe dakika ya 49 na Shamiri Mohamed alifunga mawili dakika ya 52 na 55.

Kwenye mchezo uliochezwa juzi jioni kwenye uwanja wa Karume Polisi Morogoro waliifunga Azam bao 1-0

Mchezo huo ulikuwa wa ushindani sana kila timu ikitafuta bao kwa hali na mali lakini dakika ya 80 Polisi Morogoro walipata bao baada ya kutokea piga na nikupige langoni kwa Azam.

Bao hilo lilifungwa na Benja Ngasa kwa shuti la karibu na go

No comments:

Post a Comment