Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, November 12, 2012

AVB AJITWISHA ZIGO LA LAWAMA




ANDRE Villas-Boas, amesema yeye ndiyo anastahili lawama baada ya timu yake ya Tottenham Hotspurs, kupoteza nafasi ya kuwafunga mabingwa wa Ligi Kuu ya England, Manchester City, na kujikuta wakilala kwa mabao 2-1.
Tottenham walionekana kuwa na nafasi ya kushinda pambano hilo baada ya kuanza kufunga kupitia kwa Steven Caulker katika dakika za mwanzo za kipindi cha kwanza.
Lakini AVB amekiri kwamba kocha wa Man City, Roberto Mancini alifanya mabadiliko sahihi katika kipindi cha pili cha mchezo huo na kuamua kutumia mabeki watatu.
AVB alishindwa kujibu mapigo na kujikuta akilala kwenye pambano hilo baada ya Sergio Aguero kuirudisha Man City mchezoni na supa sub Edin Dzeko akafunga bao la ushindi.
Kocha huyo alisema kwamba wakati matokeo yakiwa 1-1 aliamua kupaki basi ilikupata sare lakini kitendo hicho kiliwapa nafasi Man City kuwashambulia sana kitu kilichoamsha mashabiki, na kufanya mechi kuwa ngumu kwao kutokana na mashambulizi mfululizo ya Man City mpaka pale Dzeko alipofunga bao la ushindi

No comments:

Post a Comment