
Shinikizo hilo linafuatia mwanzo wenye ufanisi mkubwa katika mechi zake za ligi kuu ya uropa na ile ya uingereza dhidi ya Arsenal ambapo kijana huyo alifunga mabao mawili.
Kulingana nao mchezaji huyo aliyefufua matumaini ya Manchester United msimu huu anapaswa kutambuliwa na kupewa hadhi ya juu anayostahili katika programu hiyo ya FIFA 2016.
Kocha wa Man United Louis Van Gaal alimsifu kwa ''kipaji chake cha kipekee''.
Sasa mashabiki wake wanataka kampuni inayoitengeneza programu hiyo waimarishe hadhi yake.
Katika programu hiyo kwa sasa Rashford amepewa hadhi ya mchezaji wastani na jumla ya alama 59 (ambayo sio nzuri ya kutosha kwa mujibu wa wafuasi wa klabu hicho cha Manchester United).
Mmiliki mmoja wa programu hiyo ya FIFA 2016 ernie_els alichapisha hoja kwenye mitandao akidai kuwa ''Rashford ndiye mshambuliaji nyota katika ligi kuu ya Uingereza kwa sasa'' Aidha alimfananisha mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 18 na Ronaldo na kumbatiza jina "Rashaldo".
''Aidha kasi yake ikitathminiwa kuwa kati ya 77-78% huku ubora wake ukikisiwa kupanda hadi kati ya asili mia 82-83''.
Mikey Kalinowski naye alisema kuwa ''kwa kweli ni mapema mno kumsawazisha na kigogo wa soka ya Argentina na Barcelona ya Uhispania Lionel Messi.
Hata hivyo aliendelea kusema kuwa Rashford ni mbora kumzidi Messi''
No comments:
Post a Comment