Real Madrid wapo huko Rome kucheza Leo na AS Roma katika Mechi ya Kwanza ya Raundi ya Mtoano ya UEFA CHAMPIONS LIGI.
Akiwa pamoja na Kocha wake Zinedine Zidane, Ronaldo aliulizwa ikiwa urafiki wa karibu sana wa Messi, Suarez na Neymar ndio umewafanya wafunge Bao 22 zaidi ya Mastraika wa Real, yeye, Bale na Benzema, Msimu huu, Ronaldo alijibu: "Hilo unasema wewe. Nilipokuwa Man United na Paul Scholes, Ryan Giggs na Rio Ferdinand, tulizungumza tu 'Habari za Asubuhi' na 'Usiku Mwema' na tulitisha Uwanjani!"
Alipoulizwa kuhusu Messi kupiga Penati aliyompasia Suarez na kufunga Juzi Jumapili, Ronaldo alijibu: "Najua kwa nini alifanya vile na sisemi zaidi!"
Hapo Ronaldo akatimka Ukumbini na kumwacha Kocha wake Zidane akicheka.
No comments:
Post a Comment