LEO NI MAN UNITED vs SHREWSBURY TOWN EMIRATES FA CUP
DROO ya kupanga Mechi za Raundi ya 6 ambazo ndio Robo Fainali ya Kombe Kongwe Duniani, FA CUP, ambalo sasa linaitwa EMIRATES FA CUP baada ya udhamini wa Kampuni ya Ndege ya UAE, Emirates Airlines, ilifanyika Jana huko Stamford Bridge mara baada ya Chelsea kuitwanga Man City 5-1 kwenye Mechi ya Raundi ya 5 ya Kombe hili.
Ambao kwa sasa wanasuasua kwenye Ligi 1 wakiwa Nafasi ya 19 ikiwa ni Pointi 3 tu juu ya Timu zile ziko hatarini kushuka Daraja.
Lakini nao Man United wanatinga kwenye Mechi hii kutoka kwenye vichapo viwili mfululizo toka kwa Sunderland kwenye Ligi Kuu England na FC Midtjylland kwenye EUROPA LIGI.
Shrewsbury wao wanatinga kwenye Mechi hii wakitika ushindi wa 3-2 walipocheza na Blackpool kwenye Ligi na kwenye Raundi zilizopita za FA CUP walizitoa Cardiff City na Sheffield Wednesday.
Post a Comment