Poole, mwenye Miaka 17 anaetoka Wales, alisainiwa na Man United kutoka Newport County mwanzoni mwa Msimu huu lakini akagubikwa na utata wa Kibali cha Uhamisho wa Kimataifa.
Lakini Juzi, Poole aliichezea Man United U-21 ikicheza na Everton na kusafisha njia kwa yeye kuwekwa kwenye Kikosi rasmi cha UEFA EUROPA LIGI.
Kikosi ambacho kimesajiliwa kwa UEFA kwa ajili ya EUROPA LIGI kina Wachezaji 24 lakini hakina Makinda kadhaa wakiwemo Paddy McNair, Cameron Borthwick-Jackson na Andreas Pereira kwa vile wao wanakubalika kuwekwa kwenye Listi B ya Kikosi ambayo huruhusiwa idadi yeyote ya Wachezaji Chipukizi ili mradi tu wawe wamekuzwa vipaji vyao Klabuni hapo au Nchi ambayo Klabu inatoka.
![](https://metrouk2.files.wordpress.com/2015/10/depay1-e1445340154742.jpeg?w=620&h=404&crop=1)
No comments:
Post a Comment