Ligi inaongozwa, bila kutarajiwa, na Leicester City ambao wako Pointi 5 mbele ya Timu ya Pili Arsenal na Pointi 6 mbele ya Timu ya 3 Man City.
Hali hiyo inafanya Mechi hii kuwa muhimu mno kwa nani atamkaribia na kumkimbiza Leicester City wakati Ligi ikibakisha Mechi 2 kufikia nusu ya Msimu huu wa 2015/16.
Kwa Arsenal, ushindi kwao dhidi ya City kutaleta matumaini kwao na Meneja wao Arsene Wenger ya kutwaa Ubingwa wa England ambao hawajauchukua kwa Miaka 12 sasa.
No comments:
Post a Comment