Pages

Friday, August 7, 2015

MGOSI NAHODHA MPYA SIMBA




MSHAMBULIAJI mkongwe wa Simba, Musa Hassan Mgosi ameteuliwa kuwa nahodha mpya wa timu hiyo
 Mgosi amepewa ubosi huo na Kocha Mkuu wa Simba, Muingereza, Dylan Kerr baada ya kuridhishwa na nidhamu pamoja na kiwango cha Mgosi.
Awali manahodha wa Simba walikuwa Hassan Isihaka na Jonas Mkude lakini kocha lakini kocha ameangalia mtu mzoefu zaidi na anayehamasisha wenzake.
Akizungumza jijini, Kocha msaidizi wa Simba SC, Seleman Matola amethibitisha uteuzi huo na Mgosi ameteuliwa kuwa nahodha kutokana na uzoefu mkubwa.
“Kocha ameangalia uzoefu, nahodha anatakiwa mtu kama Mgosi, anaweza kuongea na wachezaji, anahamasisha timu, ndio maana ameteuliwa”.
Pia Matola alisema timu inaweza kuwa na manahodha wanne, lakini Isihaka na Mkude wataendelea kujifunza kwa Mgosi, pindi atakapoondoka wataweza kurithi nafasi yake.

No comments:

Post a Comment