Bao la Neymar lilifungwa Dakika ya 25 baada krosi ndefu ya Messi kumkuta Jeremy Mathieu aliemshushia Neymar na kufunga.
Messi alifunga Dakika ya 40 alipolishwa vizuri na Neymar.
Bao la 3 la Barca lilifungwa Dakika ya 66 na Rakitic.
Mechi zijazo kwa Barca ni Jumanne ijayo huko Tbilisi, Geargia ambayo wao kama Mabingwa wa Ulaya watawavaa Mabingwa wa Europa Ligi Sevilla, pia ya Spain, katika Mechi maalum kuashiria Msimu mpya wa UEFA ya kugombea UEFA SUPER CUP.
Kisha Barca watarudi kwao Spain kucheza Mechi ya kufungua pazia Msimu mpya huko Spain ya kugombea Spanish Super Cup dhidi ya Athletic Bilbao anbayo huchezwa kwa mikondo miwili ya Nyumbani na Ugenini.
Barca watakutana tena na Bilbao kwenye Mechi yao ya kwanza kabisa ya utetezi wa Taji lao la La Liga hapo Agosti 23.
No comments:
Post a Comment