HII HAPA SABABU YA KASEJA KUCHAGUA KUJIUNGA NA MBEYA CITY
Kaseja amesema, kikubwa
alichoangalia kabla ya kuamua kusaini mkataba wa kuitumikia klabu ya
Mbeya City ni ushindani wa klabu atakayokwenda kucheza kwenye ligi kuu
Tanzania bara na baadae kuamua kujiunga na Mbeya City.
“Kwanza nachoweza kusema ni
kwamba, naviheshimu vilabu vyote, naiheshimu Coast, African Sports,
Ndanda, Mwadui na timu zote zinazocheza ligi kuu ni timu kubwa kwahiyo
zote naziheshimu. Nilijaribu kuwa mtulivu kwa kipindi chote hiki
kuangalia ni timu ipi nitaenda kucheza ambayo itakuwa na ushindani
mkubwa”, amesema Kaseja.
Kaseja anaesubiri kujumuishwa
kwenye kikosi cha Mbeya City amewaomba wachezaji wenzake wa kikosi hicho
pamoja na mashabiki wa timu hiyo kuwa na muungano, umoja na amani ili
kuifikisha timu yao pale ambapo kila mwana Mbeya City anataka timu hiyo
ifike.
Post a Comment