Rio Ferdinand akiwa na mtoto aliyekabidhiwa wakati wa zoezi la kusaini.
Mlinzi wa Manchester United Rio Ferdinand amekabidhiwa mtoto wakati wa zoezi la utiaji saini katika kitabu chake kipya mjini Sydney.
Anazindua kitabu hicho ambacho kitakuwa na jina la 'Rio: My Decade as a Red' in the United Kingdom uzinduzi ambao utafanyika Agosti 9 lakini mashabiki wake wa Sydney wakiwa wamepata fursa ya kukiona muonekana wake mapema.Kitabu hiki kinaelezea safari nzima ya mlinzi huyo ndani ya Old Trafford tangu ajiunge nayo ikiwa ni pamoja na maisha yake binafsi.Kina jumuisha muonekano wa mawazo ya Sir Alex Ferguson na Rio wakati ambapo kuna picha zilizo chukuliwa kutoka katika video na kujumuisha maoni ya marafiki zake mashuhuri.Kupitia katika mitandao ya mauzo mitandao ya Amazon na Waterstones, kitabu hicho kimeelezewa kama 'a visual and anecdotal gem'.
No comments:
Post a Comment