BARCELONA, Hispania
NYOTA wa Barcelona, Lionel Messi,
ameingiwa hofu ya msimu ujao kukumbana na upinzani mkali kutoka kwa mahasimu
wao, timu ya Real Madrid.
Wiki iliyopita Real Madrid
ilimtangaza Carlo Ancelotti kuwa kocha wake mpya na nyota huyo anasema kuwa
timu hiyo imepata kocha mbadala.
MADRID, Hispania
KOCHA wa timu ya Taifa ya Hispania,
Vincente del Bosque, amesema kuwa hakufurahishwa na jinsi msimu uliopita
alivyokuwa akifanyiwa mlinda mlango Iker Casillas, katika timu ya Real Madrid.
Kocha wa zamani wa Real Madrid, Jose
Mourihno, alikuwa akimsugulisha benchi
Casillas, licha ya nahodha huyo kuonekana kuwa fiti raundi ya pili.
"Nasimama upande wake," Del Bosque aliliambia
gazeti la Marca. "Watu
wanafahamu jinsi nisivyopenda kuingilia masuala ya michezo na sitaweza kufanya
hivyo, lakini nasikitika jinsi alivyofanyiwa mambo yasiyo ya kiungwana kijana
huyo wa Real Madrid,” aliongeza kocha huyo.
@@@@@@@@@@@@@@@@@
Abramovich atabiriwa kufanya makuu
Chelsea
LONDON, England
MWENYEKITI wa Chelsea, Bruce Buck, amesema
kuwa mmiliki wa timu hiyo, Roman Abramovich, anafikiria kuipatia mafanikio
mengine mengi wakati wakiingia karne ya pili akiwa mmiliki wa timu hiyo.
Katika kipindi cha miaka 10 tangu aichukue
klabu hiyo, Abramovic ameifanya kuwa moja timu tishio katika ukanda wa Ulaya.
Mwaka jana timu hiyo ilionja ladha
ya kutwaa ubingwa wa Klabu Bingwa Ulaya na kwa kufanikiwa kumrejesha Jose
Mourinho, Buck anasema kuwa raia huyo wa Russia amepanga kufanya makubwa zaidi.
No comments:
Post a Comment