Kamati
ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF) imethibitisha usajili wa wachezaji 620 kati ya 624 wa
timu za Ligi Daraja la Kwanza (FDL) inayoanza kutimua vumbi kesho
(Septemba 14 mwaka huu).
Wachezaji
wanne ambao usajili wao umezuiwa mpaka watakapokamilisha taratibu ni
Emmanuel Simwanza Namwando wa African Lyon, Godfrey Bonny Namumana
(Lipuli FC), na Enyinna Darlington na Chika Keneth Chukwu wote wa Mwadui
FC ya Shinyanga.
Darlington
na Chukwu ambao wote ni Wanigeria wamezuiwa mpaka watakapowasilisha
vibali vya kufanya kazi nchini kutoka Idara ya Uhamiaji wakati Namumana
aliyekuwa akicheza nchini Nepal bado hajapata Hati ya Uhamisho wa
Kimataifa (ITC).
Nayo
African Lyon imetakiwa kufikia muafaka na AYOSA Academy ambayo Namwando
anatoka juu ya usajili kabla ya kuanza kumtumia mchezaji huyo.
Klabu
ambazo zimemaliza nafasi zote 30 usajili katika FDL ni Friends Rangers
FC ya Dar es Salaam, na Stand United FC ya Shinyanga wakati iliyosajili
wachezaji wachache zaidi ni Burkina Faso FC. Klabu hiyo ya Morogoro
imesajili wachezaji 19 tu.
Vilevile
Kamati hiyo vilevile imethibitisha usajili wa wachezaji wanane wa klabu
za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) waliosajiliwa katika hatua ya pili ya
usajili iliyoanza Agosti 14 hadi 30 mwaka huu.
Wachezaji
hao ni Samir Ruhava na Amani Simba (Ashanti United), Robert Machucha na
Said Ndutu (Yanga U20), Ayoub Masoud na Abdallah Selemani (Coastal
Union U20), Ramadhan Kipalamoto (Simba U20) na Henry Joseph (Simba)
ambaye tayari Hati yake Uhamisho wa Kimataifa (ITC) imeshawasili.
No comments:
Post a Comment