Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, January 1, 2014

RATIBA LIGI KUU ENGLAND 2013-2014 TIMU ZOTE 20 KUTIMUA VUMBI LEO, ARSENAL KUANZA MWAKA MPYA BILA MASTAA OZIL NA GIROUD

Januari Mosi huko mwaka mpya 2014 England unaanza kwa Klabu zote 20 za Ligi Kuu kushuka dimbani ikianza Mechi ya Swansea City na Manchester City na kufuatia Mechi 8 zitakazoanza Saa 12 Jioni na Siku kufungwa kwa kimbembe cha OldTrafford kati ya Mabingwa Manchester United na Tottenham.
Man United wako Nafasi ya 6, Pointi sawa na Tottenham, wote wakiwa na Pointi 34 ikiwa ni Pointi 8 nyuma ya Vinara Arsenal lakini ni Pointi 2 tu nyuma ya Timu ya 5 Liverpool ambao nao wako Pointi 1 nyuma ya Everton walio Nafasi ya 4.


Wakati Timu zote, Man United na Spurs, zikiwa zimeanza Msimu vibaya kwa Man United kufungwa Mechi 5 kati ya 15 za kwanza za Ligi na Tottenham kumtimua Meneja wao Andre Villas-Boas, hivi karibuni Timu hizo zimeanza kufanya vizuri.

Man United wameshinda Mechi zao 6 zilizopita katika Mashindano yote wakati Tottenham, chini ya Meneja mpya Tim Sherwood, ambae hutumia Mfumo wa 4-4-2, hawajafungwa Mechi ya Ligi tangu atwae himaya Wiki mbili zilizopita.
Kwenye Mechi hii, Man United wanatarajiwa kuwa nae Wayne Rooney ambae aliikosa Mechi Jumamosi waliyowafunga Norwich City Bao 1-0 baada kupona maumivu ya Nyonga lakini huenda wakamkosa Robin van Persie, ambae, licha ya kupona majeruhi yake na kuanza Mazoezi, huenda akawa si fiti kwa Mechi baada kuwa nje Mwezi mzima.
Kieran Gibbs, Olivier Giroud, Aaron Ramsey na Mesut Ozil wote hawa watakuwa nje Arsene Wengerkazi anayo! Giroud alifunga bao la ushindi dhidi ya Newcastle juzi lakini aliumia ankle Serge Gnabry(kushoto) Lukas Podolski (katikati) na Gedion Zelalem kwenye mazoezi hivi karibuni
Serious: Santi Cazorla grins while getting a mouthful from defender Per Mertesacker
Santi Cazorla yupo pamoja na kupata maneno maneno kutoka kwa Per Mertesacker
Festive cheer: Podolski is back in the frame at Arsenal after returning from injury
Podolskinae yupo

RATIBA MECHI ZIJAZO:
Jumatano Januari 1

15:45 Swansea vs Man City
18:00 Arsenal vs Cardiff
18:00 Crystal Palace vs Norwich
18:00 Fulham vs West Ham
18:00 Liverpool vs Hull
18:00 Southampton vs Chelsea
18:00 Stoke vs Everton
18:00 Sunderland vs Aston Villa
18:00 West Brom vs Newcastle
20:30 Man United vs Tottenham

No comments:

Post a Comment