Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, October 25, 2017

TAIFA STARS KUINGIA KAMBINI NOVEMBA 5 KUIKABILI BENIN


TIMU ya soka ya Taifa, ‘Taifa Stars’ inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa dhidi ya Benin Novemba 11 mwaka huu, mjini Port Novo.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Kocha Mkuu wa Stars, Salum Mayanga alisema ameita wachezaji 21 ambao wataingia kambini  Novemba 5 kwa maandalizi ya mechi hiyo.
"Nimeita kambini wachezaji 21 lakini pia nimeita wachezaji chipukizi watatu kwa ajili ya kupata uzoefu," alisema Mayanga.  Wachezaji chipukizi walioitwa ni Yohana Nkomola, Abdul Mohamed na Dickson Job.  Taifa stars itaanza mazoezi Novemba 6 na wataondoka Novemba 9 kwenda Benin. Kikosi kamili kilichoitwa ni Makipa: Aishi Manula (Simba SC), Peter Manyika (Singida United) na Ramadhani Kabwili, mabeki ni Boniphace Maganga (Mbao FC), Abdi Banda (Baroka FC/Afrika Kusini), Gardiel Michael (Yanga), Kelvin Yondani (Yanga), Nurdin Chona (Prisons), Erasto Nyoni (Simba) na Dickson Job (Mtibwa Sugar).

Viungo ni Himid Mao (Azam FC), Hamisi Abdallah (Sony Sugar/Kenya), Muzamil Yassin (Simba), Raphael Daudi (Yanga), Simon Msuva (El Jadida, Morocco), Shiza Kichuya (Simba), Ibrahim Ajib (Yanga), Mohammed Issa (Mtibwa), Farid Mussa (Tenerife/Hispania) na Abdul Mohammed (Tusker/Kenya) na washambuliaji Mbwana Samatta (KRC Genk/Ubelgiji), Mbaraka Yussuf (Azam FC), Elias Maguri (Huru) na Yohanna Nkomola (Huru).   

No comments:

Post a Comment