Uchaguzi Mkuu wa Chama cha
Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA utafanyika Agosti 10, mwaka huu mjini
Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya
Uchaguzi), Ramadhani Mambosasa ametangaza orodha ya majina sita ya mwisho ya
wagombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi huo.
Kwa mujibu Mambosasa, wagombea
hao kwa sasa hawana budi kuendelea na kampeni hadi Agosti 9, mwaka huu.
Waliopitishwa katika orodha ya
mwisho kuwania nafasi mbalimbali za uongozi - ngazi ya taifa ni pamoja na Kidao
Wilfred, Lister Manyara, Michael Bundala, Dismas Haonga, Jamhuri Kihwelo,
George Komba, Samuel Moja na Maka Mwalwasi na Mohammed Tajdin.
Nafasi zinazowaniwa ni Mwenyekiti,
Makamu Mwenyekiti, Katibu Mkuu, Katibu Msaidizi, Mweka Hazina, Wajumbe wa
Mkutano Mkuu TFF na Wajumbe wa Kamati ya Utendaji.
No comments:
Post a Comment