Shirikisho la Mpira wa Miguu
Tanzania (TFF), imeita semina ya siku moja kwa Madaktari wa timu za Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara itakayofanyika Ijumaa Agosti 4, mwaka huu kuanzia saa 2.00
asubuhi kwenye Ukumbi wa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kwa mujibu wa Kanuni ya 73 ya
Ligi Kuu, kila klabu ya Ligi Kuu inatakiwa kuwa na daktari wa timu ambaye
pamoja na mambo mengine atahakiki afya za wachezaji na viongozi wa timu.
Kila klabu inatakiwa
kuhakikisha daktari wake anahudhuria semina hii muhimu itakayoendeshwa na
Kamati ya Tiba ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), chini ya
Mwenyekiti wake Dkt. Paul Marealle.
Bodi ya Ligi itagharamia nauli
ya basi ya kuja na kurudi Dar es Salaam kwa kila mshiriki. Tunawatakia kila la
kheri katika maandalizi ya ushiriki wa semina hiyo ambayo ni sehemu ya
maandalizi ya Ligi Kuu ya Vodacom kwa msimu wa 2017/2018.
No comments:
Post a Comment