Ligi Daraja la Kwanza Tanzania
Bara inatarajiwa kuanza Septemba 16, mwaka huu kwa timu 24 zilizogawanywa
katika makundi matatu yenye timu nane kila kundi.
Tayari TFF, ilikwisha kutangaza
makundi ya Ligi Daraja la Kwanza (FDL) kwa timu 24 zitakazochuana msimu huu wa
2017/18 kuwania nafasi tatu muhimu za kupanda daraja kucheza Ligi Kuu ya
Vodacom Tanzania Bara (VPL) msimu wa 2018/19.
Kwa mujibu wa makundi hayo
yaliyoratibiwa na Bodi ya Ligi ya TFF, kundi ‘A’ litakuwa na timu za African
Lyon, Ashanti United, Friends Rangers za Dar es Salaam, JKT Ruvu na Kiluvya
United za Pwani, Mgambo JKT ya Tanga, Mvuvumwa ya Kigoma na Polisi Moro ya
Morogoro.
Kundi ‘B’ zitakuwa timu za
itakuwa na timu za Coastal Union ya Tanga; JKT Mlale ya Ruvuma; KMC ya Dar es
Salam, Mawezi Market ya Morogoro, Mbeya Kwanza ya Mbeya, Mufundi United ya
Iringa, Mshikamano na Polisi Dar za Dar es Salaam.
Kundi ‘C’ ina timu za Alliance
School, Pamba na Toto African za Mwanza, Rihno Rangers ya Tabora, Polisi Mara ya Mara, Polisi Dodoma ya
Dodoma, Transit Camp ya Shinyanga na JKT Oljoro ya Arusha.
Kadhalika, TFF imeagiza timu za
Ashanti United, Friends Rangers, KMC na Polisi Dar ya Dar es Salaam kuwasilisha
majina ya viwanja vitakavyotumiwa na timu zao wakati wa ligi hiyo inayotarajiwa
kuanza baadaye mwezi ujao.
Kutaja viwanja hivyo ni matakwa
ya Kanuni ya 6 (1) za kanuni Mama ya VPL inayozungumzia Viwanja kadhalika
kusomwa pamoja na Kanuni ya 11 inayozungumzia Leseni za Klabu kwamba kila timu
haina budi kuwa na viwanja vya mcehi za nyumbani ikiwa ni masharti ya kupata
leseni ya klabu.
No comments:
Post a Comment