TIMU ya Kibada One imefuzu nusu fainali ya mashindano
ya Ndondo kwa penati 4-2 baada ya matokeo ya sare ya kufungana 1-1 katika dakika
90 dhidi ya Vijana Rangers katika mchezo uliochezwa Uwanja wa Kinesi Urafiki,
Dar es Salaam.
Vijana ndio walianza
kupata bao la kuongoza dakika ya kwanza likifungwa na Anuar Jabir kufuatia
shambulizi kali la kushtukiza lililofanywa baada ya kuanzishwa kwa mpira.
Kibada One
walisawazisha bao hilo dakika ya 41 kupitia kwa Selemani Mkonde baada ya mabeki
wa Vijana kusimama wakidhani ameotea bao lililodumu hadi dakika 90 na kupigiana
penalti
Akizungumza
baada ya mchezo kumalizika Waziri wa Nchi ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na
Mazingira Janury Makamba alisema soka la Tanzania linakabiliwa na changamoto
nyingi huku akipongeza vijana kujumuika kuangalia mechi hizo.
“Changamoto
kubwa ni kuendeleza soka la Tanzania, mpira unahitaji vitu vinne ili ufanikiwe
ambavyo ni vipaji, pili miundo mbinu ya mchezo ambayo ni viwanja, akademi, tatu
mifumo ya kuvumbua na kuendeleza vipaji na utawala bora katika michezo,”
alisema Makamba.
Makamba alisema
ameshuhudia mchezo mzuri sambao ulikuwa na ushindani na nguvu sawa ndio maana
mshindi amepatikana kwa penalti.
Katika
mchezo huo mchezaji wa Vijana Rangers Anwar Jabir alichaguliwa kuwa mchezaji
bora wa mechi na kuzawadiwa sh 50,000 na timu yake ikaondoka n ash 100,000 huku
Kibada One ikijichukulia sh 150,000 kutoka kwa Kampuni ya Mcheza Tanzania.
No comments:
Post a Comment