Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Monday, May 29, 2017

Everton, China wamgombea Rooney



Image result for ROONEY
MANCHESTER, England
WAYNE  Rooney ana ofa mbili za pauni milioni 50 za kujiunga na moja ya klabu za China akitokea Manchester United.
Lakini inadhaniwa Rooney atapata wakati mgumu kukataa uwezekano wa kurejea kwenye klabu iliyomkuza ya Everton pamoja na fedha nyingi kutoka klabu za China.
Maisha ya mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 31 kwenye timu ya taifa ya England yalikoma baada ya kocha wa timu hiyo Gareth Southgate kumuacha nje ya kikosi chake na sasa inaelezwa anafikiria ofa ya pauni milioni 50 kutoka China, ambapo hata kwa kiwango cha maisha ya Rooney bado hizo ni fedha nyingi.
Amejadili uwezekano wa kuhamia China na familia yake na atafanya uamuzi juu ya hatima yake wiki ijayo. Lakini ofa ya dakika za mwisho kutoka Everton inaweza kumshawishi Rooney kubaki England.
Everton  haiwezi kukaribia kiwango kikubwa cha fedha ambacho China itampa Rooney, lakini mabosi wa klabu hiyo wamedhamiria kumrejesha Rooney kwenye klabu hiyo ya tangu utoto wake.
Everton itampa Rooney mshahara wa pauni 150,000 kwa wiki kidogo zaidi ya mshahara anaolipwa na Manchester United atapoachana na klabu hiyo aliyoshinda nayo mataji 13. Mshahara wake kwa China utakuwa pauni 480,000 kwa wiki.
Rooney alisema: “Kuna ofa nyingi mezani, kwa England na nje ya England na hakika hizo ndizo natakiwa nizifanyie maamuzi.”

No comments:

Post a Comment