Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 4, 2017

WACHEZAJI SERENGETI BOYS WAFURAHIA KUFUZU, WAPANGWA KUNDI B


WACHEZAJI timu ya soka ya Taifa ya Vijana waliochini ya miaka 17, 'Serengeti boys', wamefurahia kufuzu fainali za Vijana zitakazofanyika Gabon kuanzia April, 2.
Wakizungumza na gazeti hili jana asubuhi baada ya mazoezi yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Karume, Dar es Salaam, Yohana Mkomola alisema amefurahi kusikia Tanzania imeshinda rufaa walioikatia Congo Brazaville.
"Tuna uwezo wa kufanya vizuri hivyo kushinda rufaa tunakwenda kuonesha Afrika kuwa hatukubahatisha kufuzu bali uwezo tunao," alisema Mkomola.
Naye Mwenyekiti wa Kamati ya soka la Vijana ya TFF, Ayoub Nyenzi aliwataka wachezaji hao kuwa watulivu wakati huu bali waendelee na programu ya kocha kwa umakini.
"Kipindi hiki ni kigumu kwetu, tunatakiwa kujiandaa kwa mashindano kwani fainali zinaanza Aprili 2, hivyo umakini wetu uwe kwa makocha na kufuata kile kitakachoambiwa na makocha," alisema Nyenzi.
Tanzania imepangwa kundi B na timu za Niger, Mali na Angola kwenye fainali hizo ambazo zitaanza April 2 nchini Gabon.

Tanzania iliondolewa kwenye mbio za kufuzu na Congo Brazaville kwa faida ya bao la ugenini baada ya mchezo wa awali kushinda 3-2 nyumbani na ugenini kufungwa bao 1-0.
Tanzania kupitia Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) iliikatia rufaa Congo Brazaville kwa kumchezesha Langa-Lesse Bercy aliyekuwa amezidi umri na juzi kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) limeirejesha Tanzania kushiriki katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 baada ya kushinda rufaa yake.
TFF ilikata rufaa kupinga kuchezeshwa kwa mchezo huyo, ambapo Caf iliamuru afanyiwe vipimo vya kugundua umri wake halisi,  lakini mara mbili mchezaji huyo hakutokea



No comments:

Post a Comment