Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, February 7, 2017

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU BONDIA MATUMLA



Dar es salaam, 07/02/2017, uongozi wa taasisi ya tiba ya mifupa muhimbili [MOI] unauarifu umma kwamba bwana mohamed rashid matumla (30) alipokelewa katika chumba cha wagonjwa wa dharura MOI jana alfajiri tarehe 06/02/2017 Alipokelewa akiwa na maumivu makali ya kichwa na hali ya kupoteza kumbukumbu na fahamu Alifanyiwa uchunguzi wa kina pamoja na kupata vipimo mbalimbali ikiwemo vya CT-SCAN ya ubongo ambapo tulibaini kuwa amepata jeraha kichwani na kwenye ubongo ambalo limepelekea damu kuvilia kwenye ubongo kitaalamu (Acute subdural hematoma) na kusababisha Mgandamizo kwenye ubongo upande wa kulia ambapo alihitaji upasuaji wa haraka na wa dharura, baada ya vipimo jana saa 3 asubuhi bwana mohamedi matumla aliingizwa katika chumba cha upasuaji kwa ajili ya upasuaji mkubwa wa ubongo (craniotomy)na kuondoa damu iliyo vilia kichwani. Aidha, tunapenda kuwaarifu kwamba upasuaji huo ulifanyika kwa mafanikio makubwa na ulifanywa na jopo la wataalamu wetu wazalendo 5 kwa muda wa masaa 3 Baada ya upasuaji huo tumejiridhisha kwamba bw mohamed matumla yuko salama na ameondolewa kwenye hatari ya kupoteza maisha, pamoja na mambo mengine, Taasisi ya MOI inapenda kuwataarifu watanzania na wapenzi wa mchezo wa ndondi kwamba mohamed matumla ataweza kurudi katika hali yake ya kawaida katika kipindi cha miezi 8 hadi 12 ambapo ataweza kucheza mchezo wa ngumi baada ya kupata kibali maalumu cha daktari IMETOLEWA NA KAIMU MKURUGENZI MTENDAJI MOI DR,OTHMAN KILOLOMA 7TH FEBRUARY 2017

No comments:

Post a Comment