Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 4, 2017

MWANKEMWA NA SHAURI WATAMBIANA



MABONDIA Meshack Mwankemwa wa Mbeya na Ramadhani Shauri kila mmoja ametamba kumpiga mwenzake kwa KO kwenye pambano lao la raundi kumi, ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati utakaochezwa kesho katika Uwanja wa Ndani wa Taifa, Dar es Salaam.

Wakizungumza na waandishi wa habari, Mwankemwa alisema hajaja Dar es Salaam kushangaa ghorofa bali amekuja kuonesha namna ngumi zinavyopigwa.

"Sina maneno kazi yangu ni ulingoni, naamini nitashinda kwa KO ya mapema ili kudhihirisha ngumi zipo pia mikoani hasa Mbeya," alisema Mwankemwa.

Naye bondia Shauri alisema jogoo wa shamba siku zote hawiki mjini maana hajui muda gani ni asubuhi au ni usiku hivyo atampiga kipigo cha mwana ukome.

"Huku mjini jogoo wa shamba hawiki hivyo kipigo nitakachompa hatakwenda kukihadithia hata kwa watoto wake," alisema Shauri.

Promota wa pambano huo Sadick Kinyogoli aliwataka mashabiki kufika kwa wingi kujionea mpambano huo ambao utasindikizwa na mapambano mengine mengi ya kimataifa na ya nyumbani.

"Mashabiki wa ngumi waje kwa wingi kujionea mapambano haya kwani kuna mabondia wenye vipaji," alisema Kinyogoli.

Mabondia watakaosindikiza pambano hilo ni Mohamed Matumla ambaye atapambana na Mfaume Mfaume, bondia Iddi Mkwela ataoneshana umwamba na Manyi Issa pambano la raundi kumi zisizokuwa na ubingwa.

Pambano lingine la ubingwa wa taifa utakuwa kati ya Said Chino na Twalib Tuwa ubingwa wa taifa wa TPBC, mkanda ambao unatetewa na Tuwa.

Husein Pendeza wa Ashanti Boxing clab ya Ilala atakaevaana na Said Hamdani kutoka Mbezi Conetion na Mbwana Matumla atazichapa na Suleimani Shabani

Pia kutakuwepo na pambano la kimataifa wa kina dada Anisha Bashir kutoka Malawi na Ester Boazi Kazeba wa Tanzania

No comments:

Post a Comment