Mabondia Meshack Mwankemwa wa Mbeya na Mbwana Matumla wakioneshana umwamba wa kutupiana makonde wakati wa mazoezi ya kujiandaa na mapambano yao yatakayofanyika Feb 5 katika ukumbi wa uwanja wa ndani wa Taifa Mwankemwa atapanda ulingoni na Ramadhan Shauri. |
Bondia
Meshack Mwankemwa wa Mbeya ameingia Dar es salaam kwa ajili ya mpambano wake na
Ramadhani Shauri mpambano utakaokuwa wa raundi kumi za ubingwa wa EAST/ CENTRAL
AFRICA Feb 5 katika uwanja wa ndani wa Taifa Akizungumza na waandishi wa habari
Promota wa mpambano huo Sadick Kinyogoli amesema kuwa huu ni wakati wa mwisho
wa kuelekea mpambano utafanyika mwishoni mwa wiki hii
Aliongeza
kwa kusema Mwankemwa ametuwa mwishoni mwa wiki iliyopita na Shauri ndio kwao
hivyo mpambano utakuwa mkali sana kwa kuwa mabondia wote wameshacheza mapambano
makubwa ya kimataifa hivyo wapenzi waje kuangalia burudani ya masumbwi
walioikosa kwa kipindi cha nyuma
Kinyogoli alisema
kuwa bondia Mohamed Matumla atapambana na Mfaume Mfaume wakati bondia chipukizi
Iddi Mkwela ataoneshana umwamba na Manyi Issa mpambano wa raundi kumi
zisizokuwa na ubingwa
Mchezo
mwingine wa ubingwa wa taifa utakuwa kati ya Said Chino na Twalib Tuwa ubingwa
wa taifa wa TPBC mkanda ambao unatetewa na Tuwa Husein Pendeza wa Ashanti Boxing club ya
Ilala atavaana na Said Hamdani kutoka Mbezi Connetion na Mbwana Matumla atazichapa na Suleimani Shabani
Pamoja na mpambano
mwingine wa kimataifa wa kina dada Anisha Bashir kutoka Malawi na Ester Boazi
Kazeba wa Tanzania
Aliongeza kwa kusema kuwa mabondia wote watapima
uzito pamoja na Afya zao kesho katika hotel ya Atrium iliyopo sinza Afrika sana
No comments:
Post a Comment