Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Saturday, February 4, 2017

MKOMOLA MAMBO SAFI ETOILE


MSHAMBULIAJI kinda wa Tanzania ambaye anacheza timu ya Taifa ya Vijana waliochini ya miaka 17, 'Serengeti boys', Yohana Mkomola amefuzu majaribio kwenye klabu ya Etoile du Sahel


Akizungumza na gazeti hili kwenye kambi ya Serengeti boys, Mkomola alisema alipata dili la kwenda kuichezea klabu hiyo maarufu barani Afrika baada ya kumalizika kwa hatua ya makundi ya mashindano ya Vijana Afrika.

 Habari hizo ni kweli nilienda Etoile du Sahel kufanya majaribio katika timu yao ya U-20 kwa wiki mbili lakini nilifanya kwa wiki moja na nusu tu nikapata majibu kuwa nimefuzu," alisema Mkomola.

Mkomola ambaye awali alikuwa kwenye kikosi cha pili cha Azam FC aliamua kuachana nao baada ya kuona hawamwitaji.

Kwa sasa Mkomola mwenye miaka 16 yupo kwenye kambi ya Serengeti boys ambayo inajiandaa na fainali za Vijana za Afrika zitakazofanyika April baada ya kushinda rufaa.

Tanzania iliondolewa kwenye mbio za kufuzu na Congo Brazaville kwa faida ya bao la ugenini baada ya mchezo wa awali kushinda 3-2 nyumbani na ugenini kufungwa bao 1-0.

Tanzania kupitia Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) iliikatia rufaa Congo Brazaville kwa kumchezesha Langa-Lesse Bercy aliyekuwa amezidi umri na juzi kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) limeirejesha Tanzania kushiriki katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya miaka 17 baada ya kushinda rufaa yake.

TFF ilikata rufaa kupiga kuchezeshwa kwa mchezo huyo, ambapo Caf iliamuru afanyiwe vipimo vya kugundua umri wake halisi,  lakini mara kadhaa mchezaji huyo hakutokea

No comments:

Post a Comment