TIMU ya
Lipuli imekuwa timu ya kwanza toka daraja la kwanza kupanda Ligi Kuu msimu ujao
baada ya jana kuifunga Polisi Dar es Salaam mabao 3-1 kwenye mchezo uliochezwa
Uwanja wa Kumbukumbu ya Samora mjini Iringa.
Lipuli
ambayo ilicheza mbele ya mashabiki wake imeandika historia hiyo kwani tangu
1996 ndio mara ya mwisho kwa mkoa wa Iringa kushiriki ligi kuu bila kufungwa
nyumbani.
Kwa matokeo
hayo Lipuli imefikisha pointi 29 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote kwenye
kundi A huku ikiwa na michezo miwili mkononi, mmoja dhidi ya Ashanti United na
mwingine dhidi ya Pamba.
No comments:
Post a Comment