Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, February 3, 2017

KUSAFIRI KUSIKUNYIME FURSA YA KUFANYA MAZOEZI MCHONGO MZIMA HUU ....................




Je, unapenda mazoezi? Umeshawahi kujikuta ukiwa njia panda ukijiuliza aidha usafiri au la, kwa kuhofia kutopata fursa ya kufanya mazoezi? Basi ondoa shaka kwani Jumia Travel inakujulisha kuwa hoteli zifuatazo zina sehemu na vifaa vya kisasa kwa ajili ya kufanyia mazoezi.    

Ledger Plaza Bahari Beach Hotel
Hii ni hoteli ya kisasa inayopatikana katika fukwe safi za mwambao wa bahari ya Hindi, Kunduchi jijini Dar es Salaam. Licha ya kuwa na huduma mbalimbali ambazo mteja atazihitaji akiwa pale, hoteli imezingatia uwepo wa sehemu ya kufanyia mazoezi iliyosheheni vifaa vya kisasa kabisa. Lengo ni kukidhi haja ya baadhi ya wateja ambao kwao mazoezi ni sehemu ya maisha yao. Hoteli ipo karibu na mji wa Bagamoyo ambapo ni mwendo wa takribani dakika 30 na pia itakuchukua dakika 10 kusafiri kwa kutumia boti kufika kisiwa cha Mbudya.   
Jangwani Sea Breeze Resort
Hoteli hii inapatikana Tanzania bara na inajivunia kuwa na mazingira rafiki kwa watoto. Hii ni kwa sababu wanaweza kwenda na wazazi wao huku wakipatiwa chumba chenye michezo mbalimbali kwa ajili yao. Ukiwa pale itakuchukua mwendo wa dakika 10 kwa boti kufika katika visiwa vya Mbudya na Bongoyo wakati kufika mji wa kihistoria wa Bagamoyo ni takribani dakika 40 tu. Hoteli hii nayo ina sehemu na vifaa vya kufanyia mazoezi, hivyo kuwatoa hofu wapenda mazoezi pindi wakiwa pale.   

Harbour View Suites
Kama unapenda kufurahia mandhari nzuri ya katikati ya jiji la Dar es Salaam, Harbour View Suites itakuwa ni chaguo sahihi kwako. Hoteli hii ya kifahari yenye nyota nne ina sehemu yenye vifaa vya kutosha kwa ajili ya mazoezi, sehemu ya kuogelea pamoja na ‘kasino.’ Ni sehemu nzuri kufikia na kupumzika kama una shughuli za kibiashara katikati ya mji kwa sababu ipo karibu na ofisi muhimu pamoja na kumbi za mikutano.

Mermaids Cove Beach Resort & Spa
Mbali na huduma nzuri utakazozikuta pale, hoteli hii inayopatikana katika fukwe safi za Pwani ya Mashariki mwa visiwa vya Zanzibar, inazo shughuli mbalimbali za kukufanya uburudike. Ikiwa na chumba kilichotengenezwa maalumu kwa michezo mbalimbali pia ina sehemu ya kufanyia mazoezi. Kwa kuongezea ina ukumbi wa mikutano, sehemu ya kupumzika pamoja na duka kwa ajili ya manunuzi madogo madogo ukiwa hotelini. 
Hii inaweza kuwa changamoto kwa wamiliki wa hoteli kutakiwa kuzingatia kutengeneza sehemu ya mazoezi pamoja na kuweka vifaa vya kisasa. Kutokuwa na huduma hii licha ya kuwa na nyinginezo inaweza ikawa ni sababu ya wateja kutochagua kufikia kwenye hoteli yako.
Tembelea dream deals ili kujionea ofa kabambe za namna ya kwenda kufurahia huduma kwenye hoteli zilizoorodheshwa hapo juu pamoja na zifuatazo: Hotel White Sands: The Beach Resort, Golden Tulip Hotel na Ramada Resort za Dar es Salaam; Paradise Beach Resort na Golden Tulip Zanzibar Boutique Hotel za Visiwani Zanzibar; Nashera Hotel (Morogoro), Kwetu Hotel (Tanga); na Ngare Sero Mountain Lodge (Arusha)  


No comments:

Post a Comment