KAMATI ya
Utendaji ya Shirikisho la Soka la Afrika (Caf) limeirejesha Tanzania kushiriki
katika fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kwa vijana wenye umri chini ya
miaka 17 baada ya kushinda rufaa yake.
Shirikisho
la Soka Tanzania (TFF) lilimkatia rufaa mchezaji wa Congo Brazzaville,
Langa-Lesse Bercy aliyechezeshwa baada ya kuzidi umri.
Katika
mchezo wa mwisho kabla ya kufuzu, Serengeti Boys ilishinda bao 3-2 jijini Dar
es Salaam kabla ya kufungwa 1-0 na kutolewa kwa faida ya bao la ugenini.
TFF ilikata
rufaa kupiga kuchezeshwa kwa mchezo huyo, ambapo Caf iliamuru afanyiwe vipimo
vya kugundua umri wake halisi, lakini
mara kadhaa mchezaji huyo hakutokea.
Waziri wa
Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Nape Nnauye jioni hii alikaririwa na Radio ya
TBC Taifa, ambapo alithibitisha kuwa, Tanzania imeshinda rufaa yake na sasa
itashiriki fainali hizo za Mataifa ya Afrika kwa vijana yatakayofanyika baadae
mwaka huu.
Serengeti
Boys inaendelea na maandalizi ya mashindano katika hostelini za TFF zilizopo
Karume tayari kushiriki mashindano.
Tanzania
iliondolewa kushiriki katika fainali za mwaka 2005 zilizofanyika Gambia baada
ya kumchezesha Nurdin Bakari aliyezidi umri.
No comments:
Post a Comment