Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, January 13, 2017

RAIS MALINZI AMPONGEZA MKURUGENZI SINGO

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Bw. Jamal Malinzi amempongeza Bw. Yusuph Singo Omari kuteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Idara ya Maendeleo ya Michezo Tanzania.
Mapema wiki hii, Yusuph Singo Omari, aliteuliwa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Nape Moses Nnauye kushika wadhifa huo kujaza nafasi iliyoachwa wazi na Leonard Thadeo aliyehamishiwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi.
Kabla ya uteuzi huo uliofanywa kwa mujibu wa Sheria ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2002 kifungu namba 6, kifungu (1) (b) kikisomwa pamoja na kifungu namba 8 cha sheria hiyo, Bw. Yusuph Singo Omari alikuwa Mkufunzi Mwandamizi katika Chuo Kikuu cha Ardhi katika masuala ya Michezo.
Katika pongezi zake, Rais Malinzi amepokea wito wa Waziri Nape Nnauye kumpa ushirikiano wa kutosha kwa Yusuph Singo Omari atakapokuwa anatekeleza majukumu yake.
“Sisi wa TFF tunakupongeza kwa nafasi hiyo, tunachukua nafasi hii kukuahidi kukupa ushirikiano wa kutosha katika majukumu yako mapya. Hii ni kuitikia wito wa Waziri Nape ambaye aliomba wanafamilia yote ya michezo kukupa ushirikiano,” alisema Malinzi alipozungumza na mtandao wa www.tff.or.tz.
Rais Malinzi alisema kwamba program za TFF kwa sasa kwa timu zake zote za taifa, hazina budi kuungwa mkono na Serikali ili kufanikisha na kiungo mkubwa katika eneo hilo ni Bw. Yusuph Singo Omari ambaye ndiye mkuu wa Idara ya Maendeleo ya michezo – mpira wa miguu ukiwa ni miongoni mwa michezo hiyo.

No comments:

Post a Comment