Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, January 10, 2017

CBE YATETEA KOMBE LA MASHINDANO YA VYUO SOKA LA UFUKWENI




Mkuu wa Biashara Kanda ya Dar es salaam wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Jane Mwakalebela (wa tatu kushoto) akimkabidhi nahodha wa timu ya Chuo cha Elimu ya Biashara Dar es Salaam (CBE), Ally Rabi (wa tatu kulia) fedha shs 600,000/- pamoja na laini za TTCL za 4G LTE zenye muda wa maongezi wa simu na intaneti (10GB) kwa muda wa mwezi mmoja baada ya kuibuka washindi wa Mashindano ya Mpira wa Miguu wa Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer'. CBE ilikifunga Chuo cha Ardhi mabao 2-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika Ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es Salaam.

Wachezaji wa timu ya Chuo cha Elimu ya Biashara Dar es Salaam (CBE), wakiwa katika picha ya kumbukumbu na Mkuu wa Biashara Kanda ya Dar es salaam wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Jane Mwakalebela (wa nne kushoto) mara baada ya kukabidhiwa zawadi ya fedha shs 600,000/- pamoja na laini za TTCL za 4G LTE zenye muda wa maongezi wa simu na intaneti (10GB) kwa muda wa mwezi mmoja baada ya kuibuka washindi wa Mashindano ya Mpira wa Miguu wa Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer'. CBE ilikifunga Chuo cha Ardhi mabao 2-0 katika mchezo wa fainali uliofanyika Ufukwe wa Coco Beach jijini Dar es Salaam.
Meneja Uhusiano wa TTCL, Nicodemus Mushi (wa pili kushoto mbele) akizungumza kwa niamba ya Kaimu Afisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Waziri W. Kindamba kwenye hafla ya uzinduzi wa mashindano ya Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' yaliofanyika jijini Dar es Salaam kwenye ufukwe wa Coco Beach na kushirikisha vyuo mbalimbali vya jijini Dar es Salaam. Wa kwanza kulia ni Mkuu wa Biashara Kanda ya Dar es Salaam wa Kampuni ya  TTCL, Jane Mwakalebela akiwa katika uzinduzihuo.

Mkuu wa Biashara Kanda ya Dar es salaam wa Kampuni ya Simu nchini Tanzania (TTCL), Jane Mwakalebela (katikati) akimkabidhi kiasi cha fedha shilingi laki nne (400,000/-) pamoja na laini za TTCL za 4G LTE zenye muda wa maongezi wa simu na intaneti (5GB) kwa muda wa mwezi mmoja nahodha wa timu ya Chuo cha Ardhi (kulia) baada ya kuibuka washindi wa pili wa Mashindano ya Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' yaliyoshirikisha vyuo mbalimbali vya jijini Dar es Salaam chini ya uratibu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Nchini (TFF). Mashindano hayo yalifanyika Ufukwe wa Coco Beach jana. Kulia ni Bw. Dimo Dibwe muandaaji wa mashindano hayo.
Baadhi ya waamuzi wa Mashindano ya Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' yaliyoshirikisha vyuo mbalimbali vya jijini Dar es Salaam wakijadiliana jambo kabla ya mechi kuendelea.
Mapambano mbalimbali ya mechi za Mashindano ya Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' yakiendelea.
Mapambano mbalimbali ya mechi za Mashindano ya Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' yakiendelea.
Mapambano mbalimbali ya mechi za Mashindano ya Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' yakiendelea.
Mapambano mbalimbali ya mechi za Mashindano ya Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' yakiendelea.

Wakati mashindano hayo yakiendelea wanafunzi wa vyuo waliendelea kujishindia zawadi mbalimbali. Kushoto ni Ofisa Masoko wa TTCL, Eric Muganda akimkabidhi vocha ya muda wa maongezi wa thamani ya shs10,000/- baada kushinda moja ya michezo iliyoambatana na zawadi kwa wanafunzi waliokuwa wakishiriki mashindano ya soka la ufukweni. 
Baadhi ya timu zilizoshiriki Mashindano ya vyuo Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' zikishangilia baada ya kushinda mechi za awali.
Mbwembwe za mabingwa...! Mabingwa wa Mashindano ya Vyuo Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' wakiwa katika moja ya pozi mara baada ya kutangazwa kuwa mabingwa.
Kikosi cha Timu ya Chuo cha Ardhi ambao waliibuka washindi wa pili katika Mashindano ya Soka la Ufukweni 'TTCL Inter College Beach Soccer' yaliyoshirikisha vyuo mbalimbali vya jijini Dar es Salaam wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa TTCL ambao ni wadhamini wa mashindano hayo.

No comments:

Post a Comment