Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, July 20, 2016

TFF KUTOA MADAWATI 200 KUCHANGIA ELIMU

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), linatarajia kutoa madawati 200 ikiwa ni sehemu ya mapato ya Ngao ya Hisani utakaochezwa Agosti 17, 2016.

Akizungumza na wandishi wa habari, Afisa habari wa TFF, Alferd Lucas, alisemna TFF inaunga mkono juhudi za Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na juhudi za Serikali kwa katika kuhakikisha vijana wa Kitanzania wanakuwa na mazingira bora ya kupata elimu.

“TFF imeona umuhimu wa kusaidia elimu ya Tanzania ndio maana imeamua
kutoa sehemu ya mapato yake kama mchango wa kusaidia madawati kupitia mchezo wa ngao ya jamii utakaochezwa Agosti 17 kuashiria msimu mpya wa Ligi Kuu”, alisema Lucas.

Pia Lucas alisema  TFF inamshukuru Katibu Mkuu wa Bunge, Dkt. Thomas Kashililah kwa juhudi za kuendelezaa mpira wa miguu na kuutumia katika kuliletea Taifa maendeleo.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania litaendelea kushirikiana na Ofisi ya Bunge Sports Club katika kufanikisha mashindano mbalimbali hasa mchezo wa Hisani kati ya Simba Sports Club na Young African (Wabunge) utakaofanyika hapo baadaye kwa mujibu wa ratiba na uratibu wa Bunge.
Mchezo wa Ngao ya Jamii utazikutanisha Yanga na Azam FC na utachezwa Agosti 17 kwenye Uwanja wa Taifa kuashiria msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

No comments:

Post a Comment