Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Friday, July 22, 2016

MAN UNITED YATOA NAMBA ZA JEZI ZA WACHEZAJI WAO KWA MSIMU MPYA 2016/17

KLABU ya Manchester United imetangaza rasmi Namba za Jezi za Wachezaji wao kwa ajili ya Msimu Mpya wa 2016/17 wakiwamo wale Watatu wapya wao.

Kwa Wachezaji Wapya, Mchezaji wa Kimataifa kutoka Ivory Coast Eric Bailly yeye atavaa Jezi Namba 3 ambayo ilikuwa haina Mtu na Fowadi kutoka Borussia Dortmund, Henrikh Mkhitaryan, ambae ni Mchezaji wa Kimataifa wa Armenia, atavaa Jezi Namba 22.

Supastaa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic, yeye atavaa Namba maarufu Namba 9 iliyokuwa ikitumiwa na Anthony Martial ambae sasa atakuwa na Jezi Namba 11 na kumfanya Adnan Januzaj kuchukua Namba 15 badala yake.

Chipukizi wa Man United, akiwamo Shujaa aliefunga Bao la ushindi kwenye Fainali ya FA CUP, Jesse Lingard, anahama kutoka Namba 35 kwenda 14, Marcus Rashford anatoka 39 na kuivaa 19 wakati Tim Fosu-Mensah anahamia Namba 24 huku Kipa Sam Johnstone akibeba Namba 32 Mgongoni.

NAMBA ZA JEZI KWA KILA MCHEZAJI: 
1: De Gea 3: Bailly 4: Jones 5: Rojo 7: Memphis 8: Mata 9: Ibrahimovic 10: Rooney 11: Martial 12: Smalling 14: Lingard 15: Januzaj 16: Carrick 17: Blind 18: Young 19: Rashford 20: S. Romero 21: Herrera 22: Mkhitaryan 23: Shaw 24: Fosu-Mensah 25: Valencia 27: Fellaini 28: Schneiderlin 31: Schweinsteiger 32: Johnstone 33: McNair 36: Darmian 38: Tuanzebe 43: Borthwick-Jackson 44: Pereira 48: Keane

No comments:

Post a Comment