Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Tuesday, July 26, 2016

KASEJA AULA SERENGETI BOYS

KIPA wa Mbeya City, Juma Kaseja ameteuliwa kuwa kocha wa makipa wa timu ya Vijana ya soka walio chini ya miaka 17 ‘Serengeti boys’.
Akizungumza na wandishi wa habari jana, Ofisa Habari wa Shirikisho la Soka Tanzania ‘TFF’ alisema kuwa Kaseja anachukua nafasi ya kocha Mharami Mohamed ambaye atakuwa kwenye kozi ya juu ya makipa.
“Serengeti boys imeondoka leo kwenda kuweka kambi nchini Madagascar kwa ajili ya kujiandaa na mchezo wa raundi ya pili dhidi ya Afrika Kusini na Kaseja atakuwepo kwenye kocha benchi kwenye mchezo huo”, alisema Lucas.
Pia Lucas alisema kwenye kikosi hicho atakosekana pia kocha msaidizi Seba Nkoma ambaye yupo kwenye kozi ya makocha ya leseni A.
Serengeti boys itaweka kambi Madagascar kwa siku kumi kabla ya kuikabili Afrika Kusini Agosti 6 na watarudiana Agosti 21 hapa nyumbani.

Endapo Serengeti boys itafanikiwa kuitoa Afrika Kusini itapambana na timu kati ya Namibia au Congo Brazaville na ikiwa itafanikiwa kushinda itakuwa imefuzu kwenda Madagascar.

No comments:

Post a Comment