Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Wednesday, June 15, 2016

LIGI KUU ENGLAND; RATIBA MSIMU MPYA 2016/2017 YATOKA, SIKU YA KWANZA ARSENAL vs LIVERPOOL, BOURNEMOUTH vs MAN UNITED

RATIBA ya Msimu mpya wa BPL, Ligi Kuu England, imetolewa Leo na katika Mechi za kwanza kabisa hapo Wikiendi ya Agosti 13 na 14 ni Bigi Mechi Uwanjani Emirates kati ya Arsenal na Liverpool.
Meneja Mpya wa Manchester United, Jose Mourinho ataanza Ugenini na Bournemouth wakati Mpinzani wake Pep Guardiola akiwa na Man City ataanza na Sunderland Uwanjani Etihad .
Mourinho na Guardiola watapambana uso kwa uso kwa mara ya kwanza katika Dabi ya Manchester Uwanjani Old Trafford hapo Septemba 10.
Mabingwa wa Ligi Kuu England, Leicester City, wataanza utetezi wao Ugenni na Timu iliyopanda Daraja Hull City wakati Meneja mpya wa Everton Ronald Koeman akicheza na Tottenham na Bosi mpya wa Chelsea Antonio Conte ataanza na Mechi ngumu Stamford Bridge na West Ham ambao wataanza kucheza Uwanja wao wa Nyumbani mpya wa Olympic Stadium Wiki moja baadae dhidi ya Bournemouth.

MECHI ZA UFUNGUZI AGOSTI 13-14:
Arsenal v Liverpool
Bournemouth v Man Utd
Burnley v Swansea
Chelsea v West Ham
C Palace v West Brom
Everton v Tottenham
Hull v Leicester
Man City v Sunderland
Middlesbrough v Stoke
Southampton v Watford

MECHI 6 ZA KWANZA KWA TIMU 5 ZA JUU
Leicester: Hull (Ugenini), Arsenal (Nyumbani), Swansea (Nyumbani), Liverpool (Ugenini), Burnley (Nyumbani), Man Utd (Ugenini)
Arsenal: Liverpool (Nyumbani), Leicester (Ugenini), Watford (Ugenini), Southampton (Nyumbani), Hull (Ugenini), Chelsea (Nyumbani)
Tottenham: Everton (Ugenini), C Palace (Nyumbani), Liverpool (Nyumbani), Stoke (Ugenini), Sunderland (Nyumbani), Middlesbrough (Ugenini)
Man City: Sunderland (Nyumbani), Stoke (Ugenini), West Ham (Nyumbani), Man Utd (Ugenini), Bournemouth (Nyumbani), Swansea (Ugenini)

Man United: Bournemouth (Ugenini), Southampton (Nyumbani), Hull City (Ugenini), Man City (Nyumbani), Watford (Ugenini), Leicester (Nyumbani)

MVUTO:
Mourinho, ambae alitimuliwa na Chelsea Mwezi Desemba, atarudi Stamford Bridge akiwa na Man United hapo Oktoba 22 wakati Chelsea wakitua Old Trafford hapo Aprili 15.
Dabi za Merseyside kati ya Everton na Liverpool ni Desemba 17 Goodison Park na Aprili 1 huko Anfield.
Dabi ya London Kaskazini kati ya Arsenal na Tottenham ni Novemba 5 (Emirates) na Aprili 29 (White Hart Lane).

No comments:

Post a Comment