Blogroll

KWA MAWASILIANO ZAIDI TUWASILIANO KUPITIA BARUA PEPE pallangyorachel@yahoo.com AU NIPIGIE KUPITIA NAMBARI 0715187511

Pages

Thursday, March 24, 2016

VIJANA WAANDAA MSAFARA WA HISANI KWA KUTUMIA MAGARI KUPINGA UJANGILI NA KUHAMASISHA UTALII WA NDANI



Mkurungezi mtendaji wa Bongo Ride Idrisa Magesa akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) kuelezea makamilisho ya maandalizi ya msafara wa hisani wa magari uliopewa jina Bongo Ride Charity Cruise (BRCC) ambao utaambatana na kutembelea mbuga ya wanyama ya Tarangire Mkoani Arusha  ikiwa na lengo kupaza sauti kuhusu janga la ujangili na pia kuhamasisha utalii wa ndani,kulia kwake ni Meneja Mawasiliano wa BRCC Krantz Mwantepele na kushoto kwake ni Mkuu wa matukio Kelvin Edes,Pembeni yake ni Mkurungezi wa Teamtezza Kennan Richard.


Meneja Mawasiliano wa BRCC Krantz Mwantepele akiongea na waandishi wa habari kuelezea kukamilika kwa maandalizi ya msafara wa hisani wa magari uliopewa jina Bongo Ride Charity Cruise (BRCC) ) utaofanyika kuanzia tarehe 25 -27 machi ambao utaambatana na kutembelea mbuga ya wanyama ya Tarangire Mkoani Arusha  ikiwa na lengo kupaza sauti kuhusu janga la ujangili na pia kuhamasisha utalii wa ndani,kulia kwake ni Meneja Mawasiliano wa BRCC Krantz Mwantepele na kushoto kwake ni Mkuu wa matukio Kelvin Edes,Pembeni yake ni Mkurungezi wa Teamtezza Kennan Richard
Wawakilishi wa Bongo Ride charity cruise wakisikiliza kwa makini maswali ya waaandishi wa habari katika mkutano huo kuhusu kuhusu ya msafara wa hisani wa magari uliopewa jina Bongo Ride Charity Cruise (BRCC) ambao utaambatana na kutembelea mbuga ya wanyama ya Tarangire Mkoani Arusha  ikiwa na lengo kupaza sauti kuhusu janga la ujangili na pia kuhamasisha utalii wa ndani.

Meneja Mawasiliano wa BRCC Krantz Mwantepele akiteta jambo na Mkurungezi mtendaji wa Bongo Ride Idrisa Magesa wakati wa mkutano na waandishi wa habari kuelezea kukamilika kwa maandalizi ya msafara wa hisani wa magari uliopewa jina Bongo Ride Charity Cruise (BRCC) ) utaofanyika kuanzia tarehe 25 -27 machi ambao utaambatana na kutembelea mbuga ya wanyama ya Tarangire Mkoani Arusha  ikiwa na lengo kupaza sauti kuhusu janga la ujangili na pia kuhamasisha utalii wa ndani.

Mkuu wa matukio Kelvin Edes ( Wa kwanza kushoto) akifafanua jambo kwa waandishi wa habari kuhusu ya msafara wa hisani wa magari uliopewa jina Bongo Ride Charity Cruise (BRCC) ambao utaambatana na kutembelea mbuga ya wanyama ya Tarangire Mkoani Arusha  ikiwa na lengo kupaza sauti kuhusu janga la ujangili na pia kuhamasisha utalii wa ndani.

Waandishi wa habari wakiwa kwenye mkutano huo wakifuatilia maelezo ya wawakilishi  wa Bongo ride charity cruise kuhusu kukamilika kwa maandalizi ya msafara wa hisani wa magari uliopewa jina Bongo Ride Charity Cruise (BRCC) utaofanyika kuanzia tarehe 25 -27 machi ambao utaambatana na kutembelea mbuga ya wanyama ya Tarangire Mkoani Arusha  ikiwa na lengo kupaza sauti kuhusu janga la ujangili na pia kuhamasisha utalii wa ndani



Dar Es Salaam, 24 Machi 2016 Vijana wa Bongo Ride, kwa ushirikiano wa vijana wenzao wa Team Tezza na TanzaniaZalendo wanayo furaha kuwatangazia umma wa watanzania kukamilika kwa maandalizi ya msafara(cruise) wa hisani wa magari uliopewa jina Bongo Ride Charity Cruise (BRCC) ) utaofanyika kuanzia tarehe 25 -27 Machi ambao utaambatana na kutembelea mbuga ya wanyama ya Tarangire Mkoani Arusha  ikiwa na lengo kupaza sauti kuhusu janga la ujangili na pia kuhamasisha utalii wa ndani,
Ujangili hapa nchini kwa miaka ya hivi karibuni umeongezeka ikiwa ni matokeo ya mahitaji makubwa  ya pembe za ndovu,pembe za kifaru na pia ngozi ya chui na bidhaa mbalimbali za wanyamapori.
Hivi sasa biashara ya wanyamapori na rasiliamali za asili imeshika nafasi ya nne kwa biashara haramu inayowafaidisha wengi duniani,baada ya madawa ya kulevya ,silaha na usafirishaji wa binadamu inakadiliwa kuwa na thamani ya dola zaidi ya 284 billion za kimarekani.
Hali hii inatisha licha ya kuwaeimisha vijana kuwa wanaweza kuwa mabalozi wa kulinda wanyamapori pamoja na rasilimali za nchi yao,pia wanatakiwa kutuma ujumbe watu waweze kuchukua hatua kuanzia ngazi ya kitaifa mpaka kimataifa.
Akizungumza na waandishi wa habari Mkurungezi mtendaji wa Bongo Ride Idrisa Magesa amesema “ tumezindua awamu  ya tatu ya Bongo Ride Charity Cruise ikiwa ni matokeo ya kuweza kusaidia jamii.Tukiwa na washiriki zaidi ya mia 2 wa hapa nchini na zaidi ya washiriki  elfu 2 Afrika mashariki. Katika awamu yetu ya kwanza tulifanya msafara wa hisani kusaidia wagonjwa waliopata ajali katika hospitali ya Tumbi Mkoani Pwani kwa kuwapatia mashuka yakutandika pamoja na kujifunikia na pia Mwaka jana tuliweza kwenda Mkoani Morogoro na kusaidia watu waishio na virusi vya UKIMWI Morogogo (WAVUMO) ikiwa nia ni kuhamasisha amani na upendo katika nchi yetu na awamu hii tumeamua kufanya ”YOUTH AGAIST POACHING” ili kufikisha ujumbe kwa vijana wenzetu na serikali kwamba tnapinga ujangili na pia kuhamasisha utalii wa ndani kama wazalendo na wapenda maendeleo.
“Malengo yetu ni kuwa na tukio la kihistoria tukiwa na nia ya kumfanya kijana wa Kitanzania kuwa na desturi ya kutembelea vivutio vilivyomo ndani ya nchi pamoja na kuwa balozi mzuri na mzalendo wa Nchi yake” Aliongeza Magesa
Mkuu wa matukio wa Bongo Ride Kelvin Edes akiongea alisema Tunategemea kuwa na siku tatu za mbio hizi za hisani za magari kuanzia Dar es salaam kuelekea Arusha tukiwa  na washiriki  zaidi ya mia 200 kutoka mikoa mbalimbali hapa nchini. Pia tutakuwa na muda wa kuongea na vyombo vya habari, kutembelea shule na kuzunguka  katikati ya mji kuweza kuongeza uelewa juu ya janga la ujangili na kuhamasisha utalii wa ndani.
“Siku ya pili tarehe 26 tutaungana na washiriki mbalimbali wa Arusha na tutaelekea Hifadhi ya wanyama Tarangire na kujionea mambo mazuri ya hifadhi hiyo na kujifunza zaidi. Jambo hili litasaidia zaidi watu kuwapa hamasa ya kwenda kujionea vivutio vya hifadhi za ndani na kumfanya kijana  ajionee utajiri uliomo ndani ya nchi yake.
Tunaamini kabisa kasi ya kuuliwa kwa maalbino imepungua kwasababu wao wenyewe wanaweza kuzitetea nafsi zao, lakini Tembo, Kifaru na wanyama wengine wanaokumbwa na janga la ujangili hawawezi kuzitetea nafsi zao na kuomba msaada, Hivyo sisi kama vijana tumejitolea kuwa mstari wa mbele kupaza sauti zetu na kutetea haki zao kwani nao wanastahili kuishi, ”Aliongeza
Meneja Mawasiliano wa Bongo Ride  Krantz Mwantepele alinukukuliwa akisema kuwa vijana wakipaza sauti zao itaamsha matumaini kuwa imefika wakati kuwa ujangili ni jambo linalotakiwa kuchukuliwa kwa hatua za haraka kukomeshwa .
“Sisi kama vijana tunaumizwa na kuongezeka kwa matukio haya ya ujangili ,uhujumu wa rasilimali ni matukio yote yanayopangwa na watu wenye tamaa za mafanikio ya haraka  na kutamalaki kwa rushwa miongoni kwa viongozi na wanajamii.”
Pia Mkurungezi na mwanzilishi wa Team Tezza Kenan Richard aliongeza kuwa vijana wanataka sauti zao zisikilizwe, kwa maana hawataki kuwa kizazi kitakachowasimulia wajukuu zao  kuwa hawakufanya jambo lolote juu ya haya na wanaomba vijana wenzetu na viongozi wa dunia kuungana nasi ili kupinga biashara haramu ya ujangili.

No comments:

Post a Comment