Habari wadau, kwa masikitiko
makubwa naomba kuwajulisha kuwa mwanafamilia mwenzetu katika uandishi wa habari
za michezo na burudani Fred Mosha ‘Mkuu’ amefariki dunia leo katika hospitali
ya Taifa Muhimbili, Dar es Salaam alikokuwa amelazwa.
Naomba tushirikiane na familia
katika kipindi hiki kigumu. Marehemu alikuwa akiishi Mbagala Saku kwa Mkongo,
tutajulishana kadri nitakavyopata taarifa, lakini marehemu alikuwa akifanya
kazi Redio Tumaini, hivyo naamini tutapata taarifa vizuri muda si mrefu.
Ahsanteni,
Katibu Mkuu TASWA
20/02/2016
No comments:
Post a Comment