31831AD600000578-3463684-image-a-30_1456401102261
Kuna orodha ya wachezaji wengi ambao wanaweza kuwa wanamvutia kocha wa Chelsea, Jose Mourinho lakini hakukosi mmoja ambaye ndiyo ambaye anamkubali uwezo wake zaidi.
Akielezea maisha yake ya ukufunzi nchini Singapore, Mourinho alimtaja mchezaji wa zamani wa Chelsea, Frank Lampard kuwa mchezaji bora wa Ligi Kuu ya Uingereza kwa muda wote ambao amefundisha soka Uingereza.
Alisema ni ngumu kwake kumtaja mchezaji bora wa dunia sababu amefundisha wachezaji mbalimbali na walio na viwango vikubwa lakini kwa kipindi ambacho amekuwa akifundisha soka Uingereza Lampard ni bora zaidi.
lamps_1725227aKocha Jose Mourinho akiwa na Frank Lampard
“Kwa Chelsea kwa kipindi cha kwanza nilipofika nilikuwa na Frank Lampard nadhani ndiyo mchezaji bora wa muda wote wa Lligi kuu ya Uingereza,” Mourinho alikiambia kituo cha Straits Times.
“Nani ni mchezaji wangu bora? Ni ngumu kwangu kusema sababu nimefundisha baadhi ya wachezaji walio na viwango vya dunia,
“Nilienda Inter (Milan), nilikuwa na (Zlatan) Ibrahimovic, nilikuwa na (Javier) Zanetti,Madrid nilikuwa na (Cristiano) Ronaldo. Nikarudi Chelsea na nikakutana tena na wachezaji wenye viwango vya dunia,” alisema Mourinho na kuongeza.
“Kama nimekutana na wachezaji wengi na walikuwa na uwezo mzuri sio vizuri kusema huyu ni bora zaidi. Haiwezekani kushinda mataji mengi bila kuwa na wachezaji ninawaheshimu wote”