Wakati klabu ya Simba ikiwa imefanya usajili katika kipindi cha
dirisha dogo kuhakikisha inakiongezea nguvu kikosi chake, taarifa
zinadai kwamba, wachezaji hao waliosajiliwa katika kipindi cha dirisha
dogo hawataruhusiwa kucheza kwenye mchezo dhidi ya Azam FC utakaochezwaa leo kwenye Uwanja wa Taifa .
Wachezaji hao hawatacheza kwa sababu bado hawajathibitishwa na kamati
ya sheria na hadhi za wachezaji ya TFF ili waanze kuitumikia klabu hiyo
ambayo kwa kiasi kikubwa ilikuwa ina matarajio ya kuwatumia kuiangamiza Azam.
Mtendaji Mkuu wa Bodi ya Ligi, Boniface Wambura, amesema kamati ya
sheria na hadhi za wachezaji hukutana mara baada ya dirisha la usajili
kufungwa kwa ajili ya kuidhinisha usajili wa wachezaji wa Klabu ikiwa
ni pamoja na kupitia pingamizi zilizowekwa kwa wachezaji mbalimbali.
“Kanuni za usajili au kanuni za ligi zinasema klabu au timu
inamwombea usajili mchezaji kwa TFF kwani ndiyo inaidhinisha
usajili baada ya TFF kuidhinisha ndipo mchezaji anapata liseni
au mchezaji anaweza akawa ameidhinishwa lakini hata hati ya uhamisho wa
kimataifa lakini itakapofika tu acheze”, amesema Wambura.
“Lakini mpaka sasa hivi kamati ya sheria na hadhi za wachezaji ambayo
ndiyo inathibitisha usajili haijakutana kwahiyo ikikutana watu wakapata
liseni wanaweza wakacheza lakini kama hawajapata liseni ni wazi
hawawezi kucheza mpaka kamati itakapokuwa imekaa”.
Lakini kamati mpaka sasa bado haijakutana kwahiyo wachezaji wote
waliosajiliwa katika dirisha dogo hawatakuwa na uhalali wa kucheza
katika michezo ya ligi kuu Tanzania bara itakayopigwa leo na kesho.
Kwahiyo wachezaji kama Brian Majwega, Paul Kiongera na Dany Lyanga
hawatapata nafasi ya kucheza kwani hadi sasa kamati ya sheria na hadhi za
wachezaji bado haijakutana kuidhinisha uhalali wa wachezaji wote
waliosajiliwa kwenye dirisha dogo na mara nyingi kamati hukuta mara
baada ya dirisha la usajili kufungwa.
No comments:
Post a Comment